2 Wafalme 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufalme Yoasi wa Yuda(2 Sik 24.1-16)

1Yoasi alianza kutawala inchi ya Yuda akiwa na umri wa miaka saba.

2Katika mwaka wa saba wa utawala ya mufalme Yehu wa Israeli, Yoasi alianza kutawala Yuda kule Yerusalema, naye akatawala kwa muda wa miaka makumi ine akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Sibia wa Beri-Seba.

3Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.

4Hata hivyo, nafasi za kuabudu miungu kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kule.

5-6Yoasi akaita makuhani na kuwaamuru, akisema: “Kila kuhani apokee feza yote inayotolewa katika nyumba ya Yawe: ni kusema malipo ya kodi za hekalu na matoleo ya mapenzi. Azipokee kutoka kwa yeyote anayemufahamu kwa kutengeneza nyumba popote panapohitajika.”

7Lakini hata nyuma ya miaka makumi mbili na mitatu ya utawala wa Yoasi, makuhani walikuwa bado hawajatengeneza hata mabomoko ya nyumba.

8Kwa hiyo mufalme Yoasi alimwita kuhani Yehoyada na makuhani wengine na kuwauliza: “Mbona hamujatengeneza nyumba? Basi, sasa hamutapokea tena feza kutoka kwa wengine lakini zitaletwa kusudi nyumba itengenezwe.”

9Makuhani wakakubali wasipokee feza tena kutoka kwa watu. Vilevile hawakukuwa na madaraka ya kutengeneza nyumba ya Yawe.

10Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.

11Kila mara walipoona kwamba kuna feza nyingi ndani ya sanduku, mwandishi wa mufalme na Kuhani Mukubwa waliingia na kupima feza yote iliyopatikana katika nyumba ya Yawe.

12Halafu kisha kuzipima walizitoa kwa wafanyakazi waliosimamia nyumba ya Yawe, nao wakazilipa kwa waseremala na wenye kujenga waliotengeneza nyumba ya Yawe,

13kwa wajengaji na wenye kuchonga mawe, na zikatumiwa kwa kununua mbao na mawe yaliyochongwa kwa kutengeneza nyumba ya Yawe na kutimiza mahitaji mengine yote ya kazi ya kutengeneza nyumba.

14Lakini feza zake hazikutumiwa kwa kulipa kazi za kutengeneza mabeseni ya feza, makasi ya kukata tambi za mishumaa, mabakuli, baragumu, wala kwa vyombo vingine vyovyote vya zahabu au vya feza.

15Zote zilitumiwa kwa kuwalipa wafanyakazi waliozitumia kwa kutengeneza nyumba ya Yawe.

16Wafanyakazi waliosimamia kazi hii walikuwa waaminifu kabisa. Kwa hiyo hakukuwa lazima ya kuwaomba watoe hesabu ya matumizi ya feza.

17Feza zilizotolewa kwa sadaka za malipo kwa ajili ya kosa na kwa sadaka za usamehe wa zambi hazikuingizwa katika nyumba ya Yawe. Hizo zilikuwa ni mali ya makuhani.

18Wakati huo Hazaeli mufalme wa Aramu akaushambulia muji wa Gati na kuuteka. Lakini Hazaeli alipoelekea Yerusalema kusudi aushambulie,

19Yoasi mufalme wa Yuda alitwaa sadaka zote zilizotakaswa na babu zake wafalme wa Yuda: Yosafati, Yehoramu na Ahazia, na kuongeza zile zake, pamoja na zahabu yote iliyokuwa katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika nyumba ya kifalme, akazituma kwa Hazaeli mufalme wa Aramu. Naye Hazaeli akatoka Yerusalema.

20Mambo mengine ya Yoasi na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.

21Wakubwa wa serikali yake wakamwasi, wakamwuia katika uwanja wa Milo kwenye barabara inayoelekea Sila.

22Waliomwua ni Yozakari mwana wa Simeati na Yozabadi mwana wa Someri watumishi wake. Halafu wakamuzika katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi. Naye Amazia mwana wake akatawala kwa pahali pake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help