1Yawe akamwambia Musa:
2Uwaamuru Waisraeli wamutoe inje ya kambi kila mutu mwenye ukoma, kila mutu anayetokwa usaha, na kila anayekuwa muchafu kwa kugusa maiti.
3Mutawatoa inje ya kambi watu wote hawa, wanaume na wanawake, kusudi wasichafue kambi yangu ninamokaa.
4Waisraeli wakafanya hivyo, wakawafukuza inje ya kambi. Kama vile Yawe alivyomwambia Musa, ndivyo Waisraeli walivyofanya.
Malipo ya makosa5Kisha Yawe akamwambia Musa:
6Uwaambie Waisraeli kwamba: Mutu yeyote, mwanaume au mwanamuke, akimukosea mwenzake, yeye anatenda zambi mbaya mbele ya Yawe.
7Anapaswa kutubu zambi yake aliyotenda; na atatoa malipo kamilifu kwa kosa lake, akiongeza asilimia makumi mbili ya malipo hayo; atatoa malipo hayo kwa yule aliyemukosea.
8Lakini ikiwa mutu huyo amekufa na hana ndugu wa karibu ambaye anaweza kupokea malipo hayo, basi, malipo ya kosa yatatolewa kwa Yawe kwa ajili ya makuhani; malipo haya ni pamoja na kondoo dume wa upatanisho ambaye atatumiwa kwa kumufanyia upatanisho kwa ajili ya zambi yake.
9Kila sadaka ya matoleo yote matakatifu ya Waisraeli watakayomuletea kuhani, itakuwa yake.
10Na kila kitu kitakatifu cha mutu kitakuwa cha kuhani; kitu chochote mutu anachomutolea kuhani kitakuwa chake.
Maneno ya wake wasiokuwa waaminifu kwa waume zao11Yawe akamwambia Musa:
12Uwaambie Waisraeli: Kama muke wa mutu yeyote amepotoka na kukosa uaminifu kwa mume wake,
13akilala na mutu mwingine bila mume wake au mutu mwingine yeyote kujua; amejichafua ingawa hakuna mutu aliyeshuhudia kitendo chake kwa sababu hakukamatwa.
14Lakini, mume wake akiingiwa na shaka na kuwa na wivu juu ya muke wake aliyejichafua; au kama amekuwa na wivu juu ya muke wake ingawa muke wake hakujichafua,
15basi wote wawili watakwenda kwa kuhani na kupeleka sadaka inayotakiwa, ni kusema sehemu ya kumi ya unga wa shayiri; lakini bila kuitia mafuta au ubani, kwa sababu ni sadaka ya vyakula ya mume anayekuwa na wivu kwa muke wake, kwa ukumbusho wa kosa.
16Kuhani atamupeleka huyo mwanamuke karibu, na kumusimamisha mbele ya Yawe.
17Kisha, atamimina maji matakatifu katika chombo cha udongo na atatwaa vumbi inayokuwa chini ndani ya hema takatifu na kuitia katika maji hayo kwa kuyafanya machungu.
18Kuhani atamuweka mbele ya Yawe na kumufunua nywele na kumupa sadaka hiyo ya vyakula inayotolewa kwa sababu ya wivu wa mume wake. Kuhani mwenyewe atashikilia kile chombo chenye maji machungu yanayoleta laana.
19Halafu kuhani atamwapisha mwanamuke huyo akisema: Ikiwa haukulala na mwanaume mwingine na kujichafua wakati uko chini ya mamlaka ya mume wako, basi, hautapatwa na laana inayoletwa na maji haya machungu.
20Lakini kama umepotoka wakati uko chini ya mamlaka ya mume wako, na kujichafua kwa kulala na mwanaume mwingine asiyekuwa mume wako,
21Yawe akuazibu hata ukuwe laana na kiapo kati ya watu wako, ukuwe tasa na tumbo lako livimbe.
22Maji haya yanayoleta laana yaingie ndani ya tumbo lako na kukufanya tasa na tumbo lako livimbe. Naye mwanamuke ataitikia: Amina! Amina!
23Kisha kuhani ataandika laana hizi katika kitabu na kuzisafisha katika maji machungu.
24Atamukunywesha mwanamuke hayo maji machungu yanayaleta laana nayo yataingia ndani yake na kumuletea maumivu makali.
25Kisha kuhani atatwaa ile sadaka ya vyakula ya wivu katika mikono ya mwanamuke huyo na kuitikisa mbele ya Yawe, na kuipeleka juu ya mazabahu.
26Halafu, atatwaa mukono mumoja wa sadaka hiyo ya vyakula kwa ukumbusho na kuiteketeza juu ya mazabahu. Kisha atamukunywesha mwanamuke maji hayo.
27Akisha kunywa, kama amejichafua na hakukuwa mwaminifu kwa mume wake maji hayo yanayoleta laana yataingia ndani ya matumbotumbo yake na kuwa machungu, na tumbo lake litavimba naye atakuwa tasa. Mwanamuke huyo atakuwa laana kati ya watu wake.
28Lakini kama mwanamuke huyo hajajichafua na hana kosa, basi hatapatwa na hasara na ataweza kupata watoto.
29Basi, hii ndiyo sheria kuelekea maneno ya wivu kama mwanamuke akiwa chini ya mamlaka ya mume wake, anapotoka na kujichafua,
30au wakati mwanaume anaposhikwa na wivu na kuwa na mashaka na muke wake. Atamusimamisha mwanamuke huyo mbele ya Yawe, na kuhani atatimiza masharti yote ya sheria hii.
31Mume wake hatakuwa na kosa lolote, lakini mwanamuke atabeba lazima ya uovu wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.