1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Mungu na mutume wa Yesu Kristo. Mimi nimetumwa kwa kuongoza watu waliochaguliwa na Mungu wapate kumwamini na kutambua ukweli unaolingana na dini yetu.
2Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.
3Alifunua neno lake kwa wakati alioupanga kwa njia ya mahubiri ambayo yeye Mungu Mwokozi wetu aliyoniamuru kutangaza.
4Ninakutumia barua hii, wewe Tito, mwana wangu wa kweli katika imani tunayoshiriki pamoja. Ninakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwokozi wetu.
Kazi ya Tito katika kisanga cha Krete5Nimekuacha katika kisanga cha Krete kusudi upate kutengeneza maneno yaliyobaki na kusimika wazee katika kanisa ndani ya kila muji, ukifuata maagizo niliyokutolea:
6muzee wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja nao watoto wake wanapaswa kuwa waamini na wasioshitakiwa neno juu ya mwenendo mubaya au juu ya kukosa utii.
7Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.
8Lakini inafaa akuwe mwenye kupenda kukaribisha wageni, mwenye kupenda mema, mukadirifu, mwenye haki, mutakatifu na mutaratibu.
9Anapaswa kushika Neno la kweli linalolingana na mafundisho yetu. Hivi ataweza kuwaonya watu kwa njia ya mafundisho ya kweli na kuwashinda wale wanaomupinga.
10Kufuatana na hiyo, kuna watu wengi hasa kati ya Wayuda walioamini, wanaokuwa waasi, wakatetea na wadanganyifu.
11Inafaa kuwanyamazisha watu hao kwa sababu wanapotosha jamaa nzima kwa kufundisha mambo yasiyofaa wakitafuta kupata mali kwa njia mbaya.
12Na hata mumoja wa manabii wao wenyewe, Mukrete, alisema: “Wakrete ni wasema uongo siku zote, nyama wabaya, wavivu na walafi.”
13Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.
14Na zaidi ya ile hawatafuata hadisi za uongo za Kiyuda wala maagizo ya watu waliopotoka mbali na ukweli.
15Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.
16Wanajidai kwamba wanamujua Mungu, lakini wanamukana kwa matendo yao. Wao ni wenye machukizo, waasi hata hawafai kwa kufanya kazi yo yote nzuri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.