1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Asafu. Wimbo.
2Mungu anajulikana katika Yuda;
jina lake ni kubwa katika Israeli.
3Makao yake ni kule Salemu;
nyumba yake ni kule Sayuni.
4Kule alivunja mishale ya waadui;
alivunja ngao, panga na silaha za vita.
5Ee Mungu, wewe unatukuzwa sana;
unajaa utukufu kuliko milima ya milele.
6Wenye nguvu wamenyanganywa,
sasa wamelala usingizi wa kifo,
washujaa wa vita hawakuweza kutumia mikono yao.
7Ulipowakaripia, ee Mungu wa Yakobo,
farasi na wapanda-farasi walipooza.
8Wewe, ee Mungu, ni wa kutisha sana!
Nani anayeweza kusimama mbele yako ukikasirika?
9Ulijulisha hukumu yako toka mbinguni.
Dunia iliogopa na kunyamaza,
10wakati ulipoinuka kutimiza hukumu,
kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.
11Kasirani ya watu inasababisha tu sifa yako;
walioponyoka katika vita watafanya sikukuu zako.
12Mumutimizie Yawe, Mungu wenu, ahadi zenu;
enyi munaokuwa karibu, mumupe zawadi Mungu wa kutisha.
13Yeye anavunja kiburi cha wakubwa;
anawatisha wafalme wa dunia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.