1Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:
2Yawe alikuja kutoka mulima Sinai,
alitutokea kutoka mulima Seiri,
aliangaza kutoka mulima Parani.
Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika,
na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.
3Yawe anawapenda watu wake,
anawalinda watakatifu wake wote.
Wanamufuata
na kupata maagizo kutoka kwake.
4Musa alituamuru tutii sheria;
ni mali ya taifa letu.
5Yawe akakuwa mufalme wa Israeli,
wakati viongozi wao walipokutana,
na makabila yote yalipokusanyika.
6Musa akasema juu ya kabila la Rubeni:
“Rubeni aishi wala asikufe,
na watu wake wasikuwe wachache.”
7Juu ya kabila la Yuda akasema:
“Ee Yawe usikilize kilio cha kabila la Yuda;
umurudishe tena kwa wandugu zake.
Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake,
usaidie kabila la Yuda mbele ya waadui zake.”
8Juu ya kabila la Lawi, akasema:
“Ee Yawe,
upatie wazao wa Lawi shauri lako,
shauri lako kwa hao waaminifu wako,
ambao uliwajaribu huko Masa.
Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.
9Walawi waliacha wazazi wao,
wakawasahau wandugu zao,
hawakuwatambua hata watoto wao,
maana walifuata amri zako,
na kushika agano lako.
10Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako;
watafundisha watu wa Israeli sheria yako.
Walawi watafukiza ubani mbele yako,
sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.
11Ee Yawe, ubariki nguvu zao,
ukubali kazi za mikono yao,
uvunje nguvu za waadui zao,
nguvu za wanaowachukia hata wasiinuke tena.”
12Juu ya kabila la Benjamina akasema:
“Hili ni kabila Yawe analopenda,
nalo linakaa salama karibu naye.
Yeye analinda muchana kutwa,
na kukaa kati ya milima yake.”
13Juu ya kabila la Yosefu akasema:
“Yawe abariki inchi yake,
kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,
14ibarikiwe kwa matunda bora yanaoiva kwa jua,
kwa matunda ya kila mwezi,
15kwa mazao bora ya milima ya kale,
na mazao tele ya milima ya kale.
16Inchi yake ijae yote yanayokuwa mazuri,
ibarikiwe kwa huruma wa Yawe,
ambaye alitokea katika kichaka.
Baraka hizi zishukie watu wa kabila la Yosefu,
aliyekuwa mukubwa kati ya wandugu zake.
17Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza,
pembe zake ni za mbogo dume.
Atazitumia kusukuma mataifa;
yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia.
Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi
na Manase kwa maelfu.”
18Juu ya kabila la Zebuluni akasema:
“Zebuluni na Isakari mufanikiwe katika shuguli zenu
na munapokuwa katika mahema yenu.
19Watawaalika wageni kwenye milima yao,
na huko watu watatolea sadaka.
Maana wao watapata utajiri wao kutoka katika bahari
na hazina zao katika muchanga wa pembeni ya bahari.”
20Juu ya kabila la Gadi, akasema:
“Atukuzwe Mungu anayemupatia Gadi sehemu kubwa.
Gadi anaikaa kama simba
akwanyue mukono na mufupa wa kichwa.
21Alijichagulia eneo zuri kuliko yote,
pahali sehemu ya kiongozi ilipotengwa.
Aliwaongoza watu na kumutii Yawe,
alitimiza mupango wa Mungu kwa Israeli.”
22Juu ya kabila la Dani akasema hivi:
“Dani ni mwana-simba
anayeruka kutoka Basani.”
23Juu ya kabila la Nafutali akasema:
“Ee Nafutali uliyeshibishwa upendeleo,
uliyejaa baraka za Yawe,
inchi yako ni mpaka kwenye ziwa Kinereti
na upande wake wa kusini.”
24Juu ya kabila la Aseri akasema:
“Aseri abarikiwe kuliko watoto wote wa Yakobo,
na upendelewe na wandugu zako wote;
na achovye muguu wake katika mafuta.
25Miji yako itakuwa ya chuma na shaba.
Usalama wako utadumu maisha yako yote!”
26Musa akamalizia kwa kusema:
“Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako,
yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia,
anapita juu katika anga katika utukufu wake.
27Mungu wa milele ndiye kimbilio lenu;
nguvu yake inaonekana katika dunia.
Aliwafukuza waadui mbele yenu;
aliwaamuru: ‘Muwaangamize.’
28Kwa hiyo, watu wa Israeli wakakaa salama,
wazao wa Yakobo peke yao,
katika inchi iliyojaa ngano na divai,
inchi ambayo anga lake linadondosha umande.
29Heri yenu ninyi Waisraeli.
Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe,
ambaye ndiye ngao ya musaada wenu,
na upanga unaowaletea ushindi!
Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu,
nanyi mutawakanyaga chini.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.