1Kisha Miriamu na Haruni wakaanza kumusema Musa vibaya kwa sababu ya mwanamuke Mukushi aliyekuwa amemwoa.
2Wakasema: Basi, Yawe amezungumuza kwa kumwagiza Musa peke yake? Si amezungumuza nasi vilevile? Yawe akasikia maneno hayo.
3(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)
4Halafu kwa rafla, Yawe akawaambia Musa, Haruni na Miriamu: Mukuje katika hema la mukutano, ninyi watatu. Basi, wote watatu wakaenda kwenye hema la mukutano.
5Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele.
6Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.
7Lakini juu ya mutumishi wangu Musa, hali ni tofauti kabisa. Yeye ana madaraka ya kuwatunza watu wangu wote.
9Hapo Yawe akawaka hasira juu yao, akaondoka, akaenda zake.
10Wingu lilipoondoka juu ya hema la mukutano, Miriamu akaonekana yuko na ukoma, mweupe kama teluji. Haruni alipogeuka na kumwangalia Miriamu, akashangaa kuona kwamba ameshikwa na ukoma.
11Hapo, Haruni akamwambia Musa: Ewe bwana wangu, tumetenda mambo ya kipumbafu na kufanya zambi. Lakini usituazibu!
12Usimufanye Miriamu akuwe kama mutu aliyezaliwa mufu, ambaye karibu nusu ya mwili wake imeozeshwa.
13Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye.
14Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi. Ang. Hes 5.2-3
15Kwa hiyo, Miriamu akafukuzwa inje ya kambi kwa muda wa siku saba. Watu hawakuanza tena safari mpaka Miriamu aliporudishwa tena katika kambi.
16Nyuma ya hayo, watu wakafanya safari kutoka Haseroti, wakapiga kambi katika jangwa la Parani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.