1Kisha Sanibalati, Tobia, Gesemi, Mwarabu na waadui zetu wengine, waliposikia kwamba tumemaliza ujenzi wa ukuta na kwamba hakuna pahali penye kubomoka (ingawa tulikuwa bado hatujaweka milango),
2Sanibalati na Gesemi wakatuma ujumbe kwangu wakisema: “Tukutane kwenye kijiji kimoja katika bonde la Ono.” Lakini walikusudia kunizuru.
3Basi, nikawatumia wajumbe, nikisema: “Kazi ninayoifanya ni ya lazima sana. Hivyo siwezi kufika kwenu kusudi kazi isipate kusimama.”
4Wakaendelea kunitumia ujumbe uleule mara ine, lakini nikawapa jibu lilelile.
5Kwa mara ya tano, Sanibalati akanitumia barua yenye kuwa wazi kwa njia ya mujumbe wake.
6Na barua yenyewe iliandikwa hivi:
Kuna habari zilizoenezwa kati ya mataifa jirani, na Gesemi anahakikisha habari hizi, kwamba wewe pamoja na Wayuda wenzako munakusudia kuasi. Hii ndiyo sababu munaujenga upya ukuta. Kulingana na habari hizo, wewe unakusudia kuwa mufalme wao.
7Kwa kuhakikisha wazo lako, umejiwekea manabii katika Yerusalema kusudi watangaze kwamba kuna mufalme katika inchi ya Yuda. Maneno haya yataelezwa kwa mufalme Artasasta. Hivyo ninashauri kwamba wewe na mimi tukutane na kuzungumuzia jambo hili.
8Nami nikamutumia jibu: “Hakuna jambo kama hilo. Habari hizo umezitunga wewe mwenyewe.”
9Walifanya hivyo kwa kututisha wakifikiri: “Hawataendelea na kazi, kwa hiyo, hakuna litakalotendeka.” Nikamwomba Mungu wangu nikisema: “Lakini sasa, ee Mungu, ninakuomba unipe nguvu.”
10Nilipokwenda kwa Semaya mwana wa Delaya mujukuu wa Mehetabeli, ambaye hakuruhusiwa kutoka kwake, akaniambia: “Twende tukutane katika nyumba ya Mungu na milango yake tuifunge kwa sababu leo usiku watakuja kukuua.”
11Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”
12Nikatambua kwamba hakutumwa na Mungu, lakini alikuwa amelipwa na Tobia na Sanibalati atangaze mabaya juu yangu.
13Alikuwa amelipwa kwa kunitisha kusudi nifanye zambi. Na kwa njia hii wangepata njia ya kuchafua jina langu kwa kunishushia heshima yangu.
14Nikamwomba Mungu nikisema: “Ee Mungu, kumbuka mambo yote Tobia na Sanibalati waliyotenda, hata yule Noadia, nabii mwanamuke, na manabii wengine waliotaka kuniogopesha.”
Kazi inakamilika15Basi, ukuta ikamalizika siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa Eluli; nayo ilidumu muda wa siku makumi tano na mbili.
16Waadui zetu katika mataifa jirani, waliposikia kwamba kazi tumeimaliza, wakaogopa na kupata haya sana; maana walijua hakika kwamba kazi hii ilikamilika kwa musaada wa Mungu wetu.
17Wakati ule wote, viongozi wa Wayuda walikuwa wakiandikiana na Tobia.
18Wengi kati ya Wayuda walishirikiana naye kutokana na kiapo chao maana alikuwa mukwe wa Sekania mwana wa Ara. Zaidi ya yote, Yehohanani mwana wake, alikuwa amemwoa binti Mesulamu mwana wa Berekia.
19Vilevile wakanielezea matendo mema ya Tobia, na wakakuwa wanamupelekea habari zangu. Naye akakuwa ananiandikia barua kwa kunitisha.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.