Mezali 29 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.

2Wenye haki wakiongozeka, watu wanafurahi. Lakini waovu wakitawala, watu wanalalamika.

3Anayependa hekima anamufurahisha baba yake; lakini anayeandamana na kahaba anapoteza mali yake.

4Mufalme akifuata sheria ya Mungu, anaimarisha inchi. Lakini akipenda kituliro, taifa linaangamia.

5Mwenye kumubembeleza jirani yake, anatega mutego wa kujinasa mwenyewe.

6Mutu mubaya ananaswa kwa kosa lake, lakini mutu wa haki anaimba na kufurahi.

7Mwenye haki anajua haki za wamasikini, lakini mutu mwovu hajui mambo hayo.

8Wenye mazarau wanaleta mavurugo katika muji muzima, lakini wenye hekima wanatuliza kasirani.

9Mwenye hekima akibishana na mupumbafu, akasirike au acheke, ni mamoja; hatatulia.

10Wanaopenda kumwanga damu wanachukia mutu mukamilifu, lakini watu wa usawa wanalinda maisha yake.

11Mupumbafu anaonyesha hasira yake wazi, lakini mwenye hekima anaizuia na kuituliza.

12Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.

13Masikini na mugandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja: wote wawili wamepewa macho na Yawe.

14Mufalme anayewaamua wamasikini kwa haki, ataona utawala wake unaimarika milele.

15Azabu na maonyo vinaleta hekima, lakini mutoto aliyeachiliwa anapatisha mama yake haya.

16Waovu wakiongozeka, zambi zinaongezeka. Lakini wenye haki watashuhudia kuanguka kwao.

17Umwazibu mwana wako naye hatakupa wasiwasi; yeye atafurahisha moyo wako.

18Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.

19Mutumwa haonyeki kwa maneno matupu; maana ingawa anayaelewa, yeye hatayatii.

20Unamwona mutu anayesema bila kufikiri? Mutu mupumbafu ni afazali kuliko yeye.

21Anayebembeleza mutumwa wake tangu utoto, kwa mwisho mutumwa yule atamurizi.

22Mwenye kasirani anachochea ugomvi, mutu wa hasira anasababisha makosa mengi.

23Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.

24Anayeshirikiana na mwizi anajizuru mwenyewe; anasikia laana ikitolewa bila kusema neno.

25Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.

26Wengi wanapenda kujipendekeza kwa mutawala, lakini mutu anapata haki yake kwa Yawe.

27Mwovu ni chukizo kwa mwenye haki, naye mwenye haki ni chukizo kwa mwovu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help