1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Toa unabii useme hivi:
Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Muomboleze na kusema: Ole kwetu siku ile!
3Kwa maana, siku hiyo imekaribia;
siku ile ya Yawe iko karibu.
Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha,
siku ya maangamizi kwa mataifa.
4Vita itakuja katika inchi ya Misri,
na wasiwasi utakuwa katika inchi ya Etiopia,
wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa,
mali zao zitakaponyanganywa,
na misingi ya miji yao kubomolewa.
5Watu wote waliofungamana na Wamisri, ni kusema watu wa Etiopia, Puti, Ludi, Uarabu yote na Libya wataangamia pamoja nao.
6Yawe anasema hivi:
Wote wanaounga Misri mukono wataangamia,
mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa,
tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
7Misri itakuwa jangwa kama inchi zinazokuwa jangwa
na miji yake itakuwa mabomoko kama vile miji iliyoteketezwa.
8Nitakapoiteketeza Misri kwa moto
na kuvunjavunja wasaidizi wake wote,
halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
9Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha
Waetiopia wanaojizania kuwa na usalama.
Watatetemeka siku Misri itakapoangamia.
Kweli! Kweli siku hiyo inakuja!
10Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Nitamutumia Nebukadneza, mufalme wa Babeli,
kwa kukomesha utajiri wa inchi ya Misri.
11Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake,
taifa la hatari kuliko mataifa yote,
watatumwa kuiangamiza inchi ya Misri.
Watachomoa panga zao juu ya Misri
na kuijaza inchi hiyo watu waliouawa.
12Nitaukausha muto Nili na vijito vyake,
na kuuzisha inchi ya Misri katika mikono ya watu waovu.
Nitasababisha uharibifu katika inchi yote
kwa mukono wa watu wageni.
Ni Mimi Yawe ninayesema hivyo.
13Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Nitaharibu sanamu za miungu,
na kukomesha miungu ya uongo ya muji wa Nofi.
Hakutakuwa mukubwa tena huko Misri.
Nitasababisha hofu itawale katika inchi ya Misri.
14Muji wa Patro nitaufanya kuwa tupu,
muji wa Soani nitauteketeza kwa moto,
nitauazibu muji wa No.
15Nitamwanga kasirani yangu juu ya Sini,
ile kimbilio inayotegemewa na Misri;
na kuangamiza makundi ya watu wa No.
16Nitateketeza inchi ya Misri kwa moto.
Sini utashikwa na wasiwasi mukubwa,
ukuta wa Nofi utabomolewa,
nao Nofi utashambuliwa na waadui muchana wazi.
17Vijana wanaume wa Oni na Pibeseti watauawa kwa upanga,
na wakaaji wengine watapelekwa katika uhamisho.
18Huko Tapanesi muchana utakuwa giza
wakati nitakapovunja mamlaka ya Misri
na kiburi chake kikubwa kitakapokomeshwa.
Wingu litaifunika inchi ya Misri
na watu wake watakamatwa mateka.
19Ndivyo nitakavyoiazibu Misri.
Na watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Kuvunjwa kwa nguvu za Misri20Siku ya saba ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na mumoja tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
21Wewe mwanadamu! Nimeuvunja mukono wa Mufalme wa Misri, nao haukutunzwa na dawa kusudi uweze kupona na kuweza kushika upanga.
22Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapingana na Mufalme wa Misri. Nitaivunja mikono yake yote miwili, ule muzima na hata ule uliovunjika. Na upanga unaokuwa katika mukono wake utaanguka chini.
23Nitawasambaza Wamisri kati ya mataifa na kuwaeneza katika inchi zingine.
24Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.
25Nitaimarisha mikono ya Mufalme wa Babeli, lakini mikono ya Mufalme wa Misri itaregea. Hapo watu watatambua kwamba mimi ni Yawe. Nitakapotia upanga wangu katika mukono wa Mufalme wa Babeli, ataunyoosha juu ya inchi ya Misri kwa kuiazibu,
26nami nitawasambaza Wamisri kati ya mataifa mengine na kuwaeneza katika inchi zingine. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.