1Kisha Elihu akaendelea kusema:
2Yobu, unaona jambo hili ni sawa?
Unasema: “Mimi ni mwenye haki mbele ya Mungu.”
3Tena unauliza: “Nimepata faida gani
kama sikutenda zambi?
Nimefaidika kuliko kama vile ningetenda zambi?”
4Mimi nitakujibu wewe
na warafiki zako vilevile.
5Basi uangalie mbingu!
Angalia mawingu yanayokuwa juu kuliko wewe!
6Ukitenda zambi, Mungu ndiye unayemuzuru?
Na kama ukizidisha makosa yako, unazani unamwumiza?
7Kama wewe ni mwenye haki, unamupatia faida,
au yeye anapokea kitu kutoka kwako?
8Uovu wako utamuzuru mwanadamu kama wewe,
haki yako itamufalia mwanadamu mwenzako.
9Kwa sababu ya mateso mengi watu wanalia,
wanaomba musaada kwa sababu ya mapigo ya wenye nguvu.
10Lakini hakuna anayesema: “Yuko wapi Mungu, Muumba wangu,
mwenye kunifanya nichangamuke usiku,
11anayetuelimisha kuliko nyama,
na kutufanya wenye hekima kuliko ndege!”
12Watu wale wanaomba musaada lakini Mungu hawajibu,
kwa sababu ya majivuno ya watu waovu.
13Kweli Mungu hasikilizi kilio cha bure;
Mungu Mwenye Uwezo hajali kilio kile.
14Atakujibu namna gani wakati wewe
unasema kwamba haumwoni
na kwamba maneno yako iko mbele yake
na wewe unamungojea!
15Sasa, kwa vile Mungu anazuia hasira yake,
wala hajali sana makosa ya watu,
16Yobu anafungua kinywa kusema maneno matupu,
anazidisha maneno bila akili.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.