1Lakini Yawe akamujibu Musa: “Sasa utaona jinsi nitakavyomutendea mufalme wa Misri. Kwa nguvu atalazimishwa kuwaacha watu wangu watoke. Kwa nguvu atawafukuza waondoke katika inchi yake.”
Mungu anamwita Musa2Mungu akamwambia Musa: “Mimi ni Yawe. ingawa sikuwajulisha jina langu, Yawe.
4Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa inchi ya Kanana ambako waliishi kama wageni.
5Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wamelazimishwa kufanya kazi za kitumwa na Wamisri, nikalikumbuka agano langu.
6Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.
7Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.
8Nami nitawapeleka katika inchi ile niliyoapa kumupa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa inchi hiyo ikuwe yenu. Mimi ni Yawe.’ ”
9Musa akawaelezea Waisraeli maneno hayo. Lakini wao hawakumusikiliza kwa sababu walikuwa wamekufa moyo kutokana na utumwa mukali.
10Kisha Yawe akamwambia Musa:
11“Kwenda kwa mufalme wa Misri, umwambie awaache Waisraeli waondoke katika inchi yake.”
12Lakini Musa akamwambia Yawe: “Angalia, Waisraeli hawanisikilizi mimi. Namna gani mufalme wa Misri atanisikia! Tena mimi ni mutu asiyekuwa na ujuzi wa kuongea!”
13Lakini Yawe akaongea na Musa na Haruni, akawaagiza waende kwa mufalme wa Misri, na kuwatoa Waisraeli kutoka inchi ya Misri.
Ukoo wa Musa na Haruni14Haya ndiyo majina ya wakubwa wa jamaa za Waisraeli. Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi. Hao walikuwa babu za jamaa za Rubeni.
15Wana wa Simeoni walikuwa: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Sauli. Huyu wa mwisho alikuwa mutoto wa mwanamuke wa Kanana. Hao walikuwa babu za jamaa za Simeoni.
16Sasa haya ni majina ya wana wa Lawi na wazao wao: Gersoni, Kohati na Merari. Lawi aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba. Ang. Hes 3.17-20; 26.57-58; 1 Sik 6.16-19
17Wana wa Gersoni walikuwa: Libuni na Simei. Hao walikuwa babu za jamaa zao.
18Wana wa Kohati walikuwa: Amuramu, Izihari, Hebroni na Uzieli. Kohati aliishi miaka mia moja makuni tatu na mitatu.
19Wana wa Merari walikuwa: Mali na Musi. Hao ndio babu za jamaa za Walawi.
20Amuramu alimwoa Yokebedi, shangazi yake, naye akamuzalia Haruni na Musa. Amuramu aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba.
21Na wana wa Izihari walikuwa: Kora, Nefegi na Zikiri.
22Wana wa Uzieli walikuwa: Misaeli, Elisafani na Sitri.
23Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.
24Nao wana wa Kora walikuwa: Asiri, Elkana na Abiasafu, ambao walikuwa babu za jamaa za Kora.
25Eleazari mwana wa Haruni, alimwoa mumoja wa wabinti za Putieli, naye akamuzalia Finehasi. Hawa ndio waliokuwa wakubwa wa jamaa za Lawi.
26Haruni na Musa ndio walioambiwa na Yawe: “Mutoe watu wa Israeli kutoka inchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.”
27Ndio haohao Musa na Haruni walioongea na mufalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli kutoka inchi ya Misri.
28Siku ile Yawe alipoongea na Musa katika inchi ya Misri,
29alimwambia: “Mimi ni Yawe. Umwambie mufalme wa Misri maneno yote ninayokuambia.”
30Lakini Musa akamwambia Yawe: “Mimi sina ujuzi wa kuongea. Mufalme wa Misri atanisikiliza namna gani?”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.