1Hizi ni mezali za Solomono: Mutoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake; lakini mutoto mupumbafu ni huzuni ya mama yake.
2Mali iliyopatikana kwa njia mbaya haifai, lakini haki inaokoa mutu kutoka kifo.
3Yawe hawaachi wenye haki wapate njaa, lakini anapinga tamaa za waovu.
4Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.
5Mwenye akili anakusanya wakati wa mavuno. Kulala wakati wa kuvuna ni haya.
6Mwenye haki anajiletea baraka yeye mwenyewe, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
7Mwenye haki anakumbukwa kwa baraka, lakini waovu watasahauliwa kabisa.
8Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
9Anayeishi kwa ukamilifu anaishi salama, lakini anayepotosha maisha yake atagunduliwa.
10Anayekonyeza macho kwa nia mbaya analeta taabu, lakini anayeonya waziwazi analeta amani.
11Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
12Chuki inaleta ugomvi, lakini upendo unafunika makosa yote.
13Katika kinywa cha mwenye ufahamu kuna hekima, lakini wasiokuwa na akili watapigwa fimbo katika mugongo.
14Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
15Mali ya tajiri ndiyo kikingio chake. Umasikini wa masikini unamuletea maangamizi.
16Mushahara wa mutu wa haki ni uzima, lakini mapato ya mwovu ni katika zambi.
17Anayekubali kufundishwa anaelekea kwenye uzima, lakini anayekataa kuonywa amepotoka.
18Anayemuchukia mwingine kwa siri ni munafiki. Anayemusingizia mutu ni mupumbafu.
19Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.
20Maneno ya mwenye haki ni kama feza bora. Akili ya mutu mwovu haifai kwa kitu chochote.
21Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.
22Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.
23Kwa mupumbafu, kutenda maovu ni kama muchezo, lakini watu wenye akili wanafurahia hekima.
24Kitu mutu mwovu anachoogopa ndicho kitakachomupata, lakini kitu mwenye haki anachotamani ndicho atakachopewa.
25Upepo mukali unapopita na mwovu anatoweka, lakini mwenye haki anaimarishwa milele.
26Kama vile siki inavyokuwa kwa meno au moshi ndani ya macho, ndivyo muvivu anavyokuwa kwa bwana wake.
27Kumwogopa Yawe kunarefusha maisha, lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28Tumaini la mwenye haki linaleta furaha, lakini tazamio la mwovu linapotea bure.
29Yawe ni kimbilio la watu wenye mwenendo sawa, lakini ataangamiza watenda maovu.
30Wenye haki hawataondolewa katika inchi hata kidogo, lakini waovu hawatakaa katika inchi.
31Kinywa cha mwenye haki kinatoa mambo ya hekima, lakini ulimi wa mutu mubaya utakatwa mbali.
32Midomo ya wenye haki inajua mambo yatakayokubaliwa, lakini vinywa vya waovu vinasema tu maovu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.