1Kisha Yobu akaendelea na masemi yake, akasema:
2Heri ningekuwa kama zamani,
wakati ule ambapo Mungu alinichunga,
3wakati taa yake iliponiangazia juu ya kichwa,
na kwa mwangaza wake nilitembea katika giza.
4Wakati ule nilifikia ukamilifu wa maisha,
wakati urafiki wa Mungu ulikaa ndani ya nyumba yangu.
5Mungu Mwenye Uwezo alikuwa angali pamoja nami,
na watoto wangu walinizunguka.
6Nyakati hizo niliogelea kwenye fanaka.
Mawe yalinitiririshia vijito vya mafuta.
7Nilipokutana na wazee kwenye mulango wa muji
na kutwaa nafasi yangu katika mukutano,
8vijana waliponiona walisimama pembeni,
na wazee walisimama wima kwa heshima.
9Wakubwa waliponiona waliacha kuzungumuza,
waliweka kidole juu ya midomo kuwaomba watu wakae kimya.
10Sauti za waheshimiwa zilinyamazishwa,
na vinywa vyao vikafumbwa.
11Kila mutu aliyesikia habari zangu alinitakia heri
na aliponiona, alikubali habari zile kuwa kweli.
12Nilimwokoa masikini aliyenililia kupata musaada,
vilevile na yatima asiyekuwa na wa kumusaidia.
13Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka.
Niliwafanya wajane waone tena furaha ndani ya moyo.
14Haki ilikuwa ndiyo nguo yangu;
kufuata sheria ya Mungu kulikuwa kama vile kanzu na taji langu.
15Kwa vipofu nilikuwa macho ya kuwaonyesha njia;
kwa viwete nilikuwa miguu yao.
16Kwa wamasikini nilikuwa baba yao;
nilifanya bidii kutetea haki za watu nisiowajua.
17Nilivunja nguvu za watu waovu,
nikawafanya wawaachilie mateka wao.
18Kisha nikafikiri: “Nitakufia ndani ya chicha yangu,”
na siku za maisha yangu zitaongezeka kama vile muchanga.
19Mimi ni kama vile muti uliotandaza mizizi ndani ya maji;
umande wa usiku unanyesha juu ya matawi yangu.
20Ninapata utukufu mupya siku zote,
na nguvu zangu tayari kama vile mushale na upinde.
21Wakati ule watu walinisikiliza na kungoja,
walikaa kimya kungojea mashauri yangu.
22Nilipomaliza kusema hawakukuwa na cha kuongeza;
maneno yangu yaliwakolea kama vile matone ya mvua.
23Watu waliningojea kama vile wanavyongojea mvua,
walikuwa kama vile watu wanaotazamia mvua ya kwanza.
24Walipokata tamaa, niliwaonyesha uso wa furaha;
walishika muchangamuko wa uso wangu.
25Niliwatangulia kwa kuwaongoza, nikawaonyesha njia.
Nilikuwa kwao kama vile mufalme kati ya majeshi yake;
kama vile mutu anayewafariji wenye musiba.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.