Yobu 41 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Yeyote anayeona yule nyama mukubwa

anakufa moyo na kuzimia.

2Hakuna mutu yeyote mukali anayesubutu kumushitua.

Nani, basi anayeweza kusimama mbele yangu?

3Nani aliyenipa kitu, kusudi nipate kumurudishia?

Chochote kinachokuwa chini ya mbingu ni changu.

4Sitaacha kukuelezea juu ya viungo vya yule nyama mukubwa

au juu ya nguvu zake na umbo lake zuri.

5Nani anayeweza kuondoa nguo yake ya inje?

Nani anayeweza kutoboa nguo ya chuma anayovaa?

6Nani anayeweza kufungua kinywa chake?

Meno yake pande zote ni kitisho!

7Mugongo wake umefanywa kwa mistari ya ngao

iliyoshikamana pamoja kama kwa muhuri.

8Kila mumoja umeshikamana na mwingine,

hata hewa haiwezi kupenya katikati yake.

9Imeunganishwa pamoja,

hata haiwezekani kuitenganisha.

10Akipiga chafya, mwangaza unatokea,

macho yake yanametameta kama jua inapotokea.

11Katika kinywa chake kunatokea mienge inayowaka,

cheche za moto zinaruka inje.

12Katika pua yake kunafuka moshi,

kama vile chungu kinachochemuka,

kama vile nyasi inayowaka.

13Pumzi yake inawakisha makaa;

ulimi wa moto unatoka ndani ya kinywa chake.

14Shingo yake ina nguvu ajabu,

nyama yule anapotokea watu wanapatwa na hofu.

15Mishipa yake imeshikamana pamoja,

imara kama chuma wala haitikisiki.

16Moyo wake ni mugumu kama jiwe,

mugumu kama jiwe la kusagia.

17Anapoinuka, mashujaa wanashikwa na woga,

kwa pigo moja wanazimia.

18Hakuna upanga unaoweza kumuumiza,

wala mukuki, mushale au nguo ya chuma.

19Kwake chuma ni laini kama unyasi,

na shaba kama muti uliooza.

20Mushale hauwezi kumukimbiza;

akitupiwa mawe ya mujeledi anayaona kama maganda.

21Kwake, gongo ni kama kipande cha bua;

anacheka akitupiwa mikuki kwa wingi.

22Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali;

anakwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kulima.

23Anatikisatikisa bahari kama maji yanayochemuka,

anaifanya itoe pofu kama chupa ya mafuta.

24Anapopita anaacha nyuma kitambulisho kinachoangaa;

pofu nyeupe inaonekana ikielea juu ya bahari.

25Katika dunia hakuna kinachofanana nayo;

hicho ni kiumbe kisichokuwa na hofu.

26Kinawaona kuwa si kitu wote wenye kiburi;

hicho ni mufalme wa nyama wote wakali.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help