Yeremia 40 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yeremia anakaa na Gedalia

1Huu ni ujumbe uliotolewa kwa Yeremia kutoka kwa Yawe wakati Nebuzaradani mukubwa wa walinzi wa mufalme alipomuruhusu Yeremia aondoke Rama. Huyo mukubwa alimukamata Yeremia akifungwa minyororo, pamoja na wafungwa wengine wote wa Yerusalema na Yuda ambao walikuwa wamepelekwa katika uhamisho kule Babeli.

2Mukubwa wa walinzi alimukamata Yeremia, akamwambia: Yawe, Mungu wako, alitangaza hasara juu ya pahali hapa.

3Na sasa Yawe ametimiza jambo hilo na kutenda kama alivyosema. Kwa sababu ninyi wote mulimukosea Yawe na kukataa kumutii, jambo hilo limewapata.

4Basi! Leo ninafungua minyororo toka mikono yako. Kama unaona ni vizuri kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi tuende pamoja; mimi nitakutunza vizuri. Lakini kama unaona si vizuri kwako kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi, usikuje. Ujue kwamba unaweza kwenda popote katika inchi hii. Basi kwenda kwenye unaona ni vizuri kwenda.

5Kama ukiamua kubaki, basi rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, ambaye mufalme wa Babeli amemusimika kuwa mutawala wa miji yote ya Yuda, ukae naye kati ya wanainchi wengine. Kama sivyo, kwenda kwenye unaona unastahili kwenda. Basi, mukubwa wa walinzi akamupa Yeremia vyakula na zawadi, kisha akamwacha ajiendee.

6Kisha Yeremia akaenda Misipa kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, akakaa naye pamoja na wanainchi waliobaki katika inchi.

7Wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori pamoja na watu wao, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, kuwa mutawala wa inchi, na kwamba alikuwa amewaweka chini ya usimamizi wake wanaume, wanawake na watoto, ni kusema watu wakosefu kabisa katika inchi ambao hawakupelekwa katika uhamisho kule Babeli,

8walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.

9Gedalia aliapa mbele yao na mbele ya waaskari wao akisema: Musiogope kuwatumikia Wakaldea. Mukae katika inchi mumutumikie mufalme wa Babeli, na mambo yote yatawaendekea vema.

10Mimi nitakaa Misipa nipate kuwa musimamizi wenu mbele ya Wakaldea watakaofika kwetu; lakini ninyi muvune matunda na mukamue divai na mafuta, mujiwekee akiba ya vitu hivyo, mukae katika miji mutakayoirizi.

11Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,

12wote walirudi kutoka pahali pote walipokuwa wametawanyika na kwenda katika inchi ya Yuda kwa Gedalia kule Misipa. Walichuma zabibu na matunda mengine kwa wingi sana.

13Basi, Yohana mwana wa Karea pamoja na wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori, walifika kwa Gedalia, kule Misipa, wakamwambia:

14Uko na habari kwamba Balisi mufalme wa Waamoni, amemutuma Isimaeli mwana wa Netania, akuue? Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuamini maneno yao.

15Kisha, Yohana mwana wa Karea akazungumuza na Gedalia kwa siri kule Misipa, akamwambia: Uniruhusu niende nimwue Isimaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu yeyote atakayejua. Kwa nini kumwachilia yeye akuue na Wayuda wote waliokusanyika hapa watawanyike na Wayuda waliobaki waangamie?

16Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu akamwambia Yohana mwana wa Karea hivi: Usifanye jambo hilo! Mambo unayosema juu ya Isimaeli si ya kweli!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help