1Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!”
Naye akaitika: “Niko hapa.”
2Mungu akamwambia: “Umutwae mwana wako, Isaka, mwana wako wa pekee unayemupenda, uende mpaka inchi ya Moria, umutoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mulima nitakaokuonyesha.”
3Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.
4Kwa siku ya tatu, Abrahamu aliinua macho akaona pahali pale kwa mbali.
5Akawaambia wale watumishi wake: “Mungoje hapa na huyu punda. Mimi na mwana wangu tutakwenda mpaka kule, tutamwabudu Mungu, kisha tutawarudilia.”
6Basi, Abrahamu akatwaa zile kuni, akamubebesha Isaka mwana wake. Yeye mwenyewe akatwaa moto na kisu katika mukono, wakaondoka pamoja.
7Isaka akamwuliza baba yake: “Baba, tuko na moto na kuni. Lakini mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa yuko wapi?”
8Abrahamu akamujibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatujalia mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.” Basi, wakaendelea na safari yao.
9Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu. kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”
15Malaika wa Yawe akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni,
16akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee, Ang. Ebr 6.13-14
17hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao. Ang. Ebr 11.12
18Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.” Ang. Mdo 3.25
19Basi, Abrahamu akawarudilia wale watumishi wake, nao pamoja wakaondoka, wakarudi Beri-Seba. Abrahamu akakaa kule Beri-Seba.
Watoto wa Nahori20Nyuma ya mambo hayo Abrahamu akapata habari kwamba Milka vilevile amemuzalia ndugu yake Nahori watoto wanaume:
21Usi muzaliwa wa kwanza, Buzi ndugu yake, Kemweli baba ya Aramu,
22Kesedi, Hazo, Pildasi, Idilafu na Betueli.
23Betueli alizaa Rebeka. Milka alimuzalia Nahori, ndugu ya Abrahamu, watoto hao wanane.
24Zaidi ya hayo, Reuma, habara ya Nahori, vilevile alimuzalia watoto: Teba, Gahamu, Tahasi na Maka.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.