1Ninasema ukweli kwa kuungana na Kristo. Na kwa uongozi wa Roho Mutakatifu zamiri yangu inanihakikishia kwamba sisemi uongo:
2mimi nina huzuni kubwa na uchungu usiokuwa na mwisho ndani ya moyo wangu.
3Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,
4ndilo taifa la Waisraeli. Wao walikubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, yeye aliwaonyesha utukufu, alifanya maagano nao, aliwapa Sheria, aliwaonyesha namna ya kumwabudu na kuwatolea ahadi zake.
5Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.
6Sisemi kwamba ahadi ya Mungu haikutimia. Kwa maana si wote wanaotoka katika uzao wa Israeli ndio Waisraeli wa kweli,
7wala si wote wanaotoka katika uzao wa Abrahamu, ndio watoto wa kweli wa Abrahamu. Kwa kuwa Mungu alimwahidia Abrahamu: “Ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.”
8Maana yake, si wale waliozaliwa sawa na kawaida wanaohesabiwa kuwa watoto wa Mungu; lakini ni wale waliozaliwa kufuatana na ahadi ya Mungu ndio wanaohesabiwa kuwa wazao wake wa kweli.
9Kwa sababu hii ndiyo ahadi ya Mungu: “Kwa wakati kama huu, nitakuja tena, na Sara atazaa mutoto mwanaume.”
10Na si vile tu; Rebeka alikuwa na watoto wawili aliowazaa na mume mumoja, ndiye babu yetu Isaka.
11-12Watoto wale walipokuwa hawajazaliwa bado, wala hawajatenda jambo lolote zuri au baya, Mungu alimwambia Rebeka hivi juu yao: “Mukubwa atamutumikia mudogo.” Alisema vile kwa kutimiza mupango wake unaotokana na uchaguzi wake usiofuatana na matendo ya watu, lakini mwito wake kwao.
13Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Nimemupenda Yakobo, lakini nimemuchukia Esau.”
14Basi tuseme nini? Mungu hafuati haki? Hapana hata kidogo!
15Kwa maana anamwambia Musa: “Nitamuhurumia yule ninayependa kumuhurumia; nitamurehemu yule ninayependa kumurehemu.”
16Basi mambo hayo, hayatokani na mapenzi ya mutu wala juhudi yake, lakini yanatokana na rehema ya Mungu.
17Mungu anamwambia mufalme wa Misri katika Maandiko Matakatifu: “Nimekusimika kuwa mufalme kwa sababu hii moja, ni kusudi kwa njia yako nipate kuonyesha uwezo wangu na kusudi jina langu lipate kutangazwa katika dunia yote.”
18Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.
Kasirani na huruma za Mungu19Labda utaniambia: “Ikiwa ni vile, sababu gani Mungu anawashitaki watu? Kwa maana hakuna anayeweza kupingana na mapenzi yake.”
20Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”
21Mufinyanzi anaweza kufanya sawa vile anavyotaka na udongo. Toka donge moja la udongo anaweza kutengeneza chombo kimoja cha heshima na kingine cha matumizi ya kawaida.
22Basi kuna nini? Mungu alitaka kuonyesha kasirani yake na kutambulisha uwezo wake. Lakini aliwavumilia sana wale waliostahili kupatwa na kasirani yake na waliokuwa wametayarishwa kwa kuangamizwa.
23Vilevile alitaka kuonyesha uwingi wa utukufu wake kwa wale aliowasikilia huruma; wale ambao alitayarisha tangu zamani kwa kuwatukuzisha.
24Ndio sisi tulioitwa naye, si toka kati ya Wayuda tu, lakini toka kati ya watu wa mataifa mengine vilevile.
25Ni vile anavyosema katika maandiko haya ya nabii Hosea:
“Wale waliokuwa si watu wangu
nitawaita sasa ‘Watu wangu.’
Taifa lile nililokosa kulipenda nitaliita sasa ‘Mupendwa wangu.’
26Na pahali pale walipoambiwa: ‘Ninyi si watu wangu!’
pale wataitwa ‘Watoto wa Mungu Mwenye Uzima.’ ”
27Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.
28Kwa maana Baba atatimiza kabisa kusudi lake juu ya dunia bila kukawia.”
29Ni kama vile Isaya alivyokuwa ametangulia kusema:
“Kama Bwana wa Majeshi hangetuponyeshea wamoja wa wazao wetu,
ingetutokea sawa Sodoma,
ingegeuka kwetu sawa Gomora.”
Waisraeli hawakufuata njia ya kuhesabiwa haki30Basi tuseme nini? Watu wa mataifa mengine waliokosa kutafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu wamehesabiwa haki mbele yake kwa njia ya imani.
31Na kwa ngambo ingine, Waisraeli waliokuwa wakitafuta Sheria kusudi kwa njia yake wapate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu, hawakuifikia.
32Kwa sababu gani? Kwa sababu walitafuta haki ile, si kwa njia ya imani, lakini kwa njia ya matendo. Walijikwaa juu ya “lile jiwe la kukwalisha,”
33kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:
“Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni
nalo ni la kuangusha.
Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.