1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Daudi.
2Ee Mungu, muteteaji wa haki yangu,
unijibu ninapoomba.
Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;
unionee huruma na kusikia maombi yangu.
3Ninyi watu, mpaka wakati gani mutachafua jina langu?
Mpaka wakati gani mutapendelea mambo ya ovyo na kusema uongo?
4Mujue kwamba Yawe amejichagulia mutu wake wa haki.
Yawe anasikia kila mara ninapomwomba.
5Mukasirike lakini musitende zambi.
Mufikiri katika vitanda vyenu na kunyamaza.
6Mutoe sadaka zinazokuwa sawa,
na kumutumainia Yawe.
7Wengi wanasema: “Heri tungefanikiwa tena!
Ee Yawe, utuangalie kwa wema!”
8Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo,
kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.
9Ninalala na kupata usingizi kwa amani;
wewe peke yako, ee Yawe, unaniweka salama.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.