1Kisha Elifasi wa inchi ya Temani, akajibu:
2Mwenye hekima anajibu bila kufikiri
na kujaa maneno ya burebure?
3Anajitetea kwa maneno yasiyofaa
na yasiyokuwa na maana?
4Lakini wewe, woga wa Mungu si ndani yako;
nawe unakataa kufikiri mbele ya Mungu.
5Uovu wako ndio unaongoza kinywa chako,
nawe unachagua kusema kama wadanganyifu.
6Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi;
masemi yako yanashuhudia juu yako.
7Wewe ndiwe mutu wa kwanza kuzaliwa?
Wewe ulizaliwa mbele ya kuwa kwa vilima?
8Ulipata kuwa katika shauri la Mungu?
Wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?
9Unajua kitu gani tusichokijua sisi?
Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
10Kati yetu kuna wazee wenye hekima,
wenye miaka mingi kuliko baba yako.
11Faraja Mungu anazokupa ni ndogo sana?
Au neno lake la upole kwako si kitu?
12Mbona moyo unakusukuma kukasirika
na kutoa macho makali,
13hata kumwasi Mungu
na kusema maneno mabaya kama yale?
14Mutu ni nini hata aweze kuwa na moyo safi?
Yule aliyezaliwa na mwanamuke atapata kuwa mwenye haki?
15Ikiwa Mungu hawaaminii hata wamalaika wake,
nazo mbingu si safi mbele yake,
16kefu sasa mwanadamu anayekuwa chukizo na mupotovu,
mwanadamu anayetenda uovu kama kunywa maji!
17Sasa unisikilize, nami nitakuonyesha,
nitakuambia yale niliyoona,
18mafundisho ya wenye hekima,
mambo ambayo wazee wao hawakuficha,
19ambao Mungu aliwapa hiyo inchi peke yao,
wala hakuna mugeni aliyepita kati yao.
20Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,
miaka yote watesaji waliyopangiwa.
21Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio.
Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.
22Mwovu hana tumaini la kutoka katika giza;
mwisho wake ni kufa kwa upanga.
23Anatangatanga kutafuta chakula,
akisema: “Kiko wapi?”
Anajua kwamba siku ya giza inamukaribia.
24Taabu na uchungu, vinamutisha;
vinamushambulia kama jeshi la mufalme anayekuwa tayari kwa vita
25kwa sababu amenyoosha mukono wake apigane na Mungu
na kujivuna kumupinga yule Mungu Mwenye Uwezo.
26Anakimbia kwa kiburi kwa kumushambulia,
akiwa na ngao yenye mafundo makubwa.
27Uso wake umenona kwa mafuta,
na kiuno chake kimenenepa.
28Ameishi katika miji iliyoachwa wazi,
katika nyumba zisizokaliwa na mutu,
nyumba zilizotakiwa zikuwe lundo la uharibifu.
29Mutu yule hatakuwa tajiri hata kidogo;
wala utajiri wake hautadumu katika dunia.
30Hataponyoka giza la kifo.
Ndimi za moto zitakausha vichipukizi vyake,
maua yake yatapeperushwa na upepo.
31Aache kutumainia udanganyifu,
maana udanganyifu ndio utakaokuwa zawadi yake.
32Atalipwa kikamilifu mbele ya kufa kwake,
na wazao wake hawatadumu.
33Atakuwa kama muzabibu unaoangusha zabibu mbichi,
kama muzeituni unaopoteza maua yake.
34Wote wasiomwogopa Mungu hawatapata watoto,
moto utateketeza mahema ya wanaokula kituliro.
35Wanatunga udanganyifu na kuzaa uovu.
Mioyo yao inapanga udanganyifu.
Jibu la YobuWho We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.