Kutoka 40 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hema linasimikwa na kutakaswa

1Yawe akamwambia Musa:

2Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimika hema takatifu la mukutano.

3Ndani ya hema hilo utaweka lile Sanduku la Agano, kisha weka pazia mbele yake.

4Utaingiza meza na kupanga vyombo vyake juu. Utaingiza kile kinara vilevile na kuweka taa zake juu yake.

5Mazabahu ya zahabu ya kufukizia ubani utaiweka mbele ya Sanduku la Agano, kisha utatundika pazia kwenye mulango wa hema takatifu.

6Ile mazabahu ya kuteketezea sadaka utaiweka mbele ya mulango wa hema takatifu la mukutano.

7Birika la kunawia utaliweka katikati ya hema la mukutano na mazabahu na kulijaza maji.

8Utazungusha upango na kutundika pazia kwenye mulango wake.

9Kisha, utatakasa hema pamoja na vyombo vyake vyote kwa kuvipakaa yale mafuta ya kupakaa, nalo litakuwa takatifu.

10Halafu, utatakasa mazabahu ya kuteketezea sadaka na vyombo vyake vyote kwa kuipakaa mafuta, nayo itakuwa takatifu kabisa.

11Birika la kunawia na tako lake vilevile utalitakasa kwa namna hiyohiyo.

12Utamwita Haruni na wana wake wakuje kwenye mulango wa hema la mukutano, kisha uwanawishe.

13Utamuvalisha Haruni zile nguo takatifu. Utamupakaa mafuta na kumutakasa, kusudi aweze kunitumikia kama vile kuhani.

14Utawaita wana wake na kuwavalisha zile kanzu.

15Kisha uwapakae mafuta kama vile ulivyomupakaa baba yao, kusudi nao vilevile wanitumikie kama makuhani. Kupakwa mafuta huku kutawaingiza katika ukuhani wa kudumu katika vizazi vyao vyote.

16Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.

17Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza mwaka wa pili kisha kutoka Misri, hema takatifu likasimikwa.

18Musa akaweka vikalio vyake, akainua mbao zake, akashikamanisha miti yake na kusimamisha nguzo zake.

19Akatandaza pazia juu ya hema takatifu na kuweka kifuniko cha hema juu yake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

20Kisha akatwaa vile vibao viwili vya mawe na kuviweka katika lile sanduku. Akapitisha ile miti katika vikomo vya sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.

21Kisha akaweka lile Sanduku la Agano ndani ya hema na kutundika pazia, na kwa namna hiyo akafunika Sanduku la Agano, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

22Akaweka meza ndani ya hema la mukutano, upande wa kaskazini, sehemu ya inje ya pazia,

23na juu yake akapanga mikate iliyotolewa kwa Yawe, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

24Akaweka kinara ndani ya hema la mukutano, upande wa kusini, kuelekea meza.

25Mule, mbele ya Yawe, akawasha taa zake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

26Akaweka ile mazabahu ya zahabu katika hema, mbele ya pazia,

27na kufukiza ubani wenye harufu nzuri juu yake, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

28Akatundika pazia kwenye mulango wa hema takatifu,

29akaweka pale kwenye mulango wa hema takatifu mazabahu ya sadaka za kuteketezwa, akatolea juu yake sadaka ya kuteketezwa kwa moto na sadaka ya ngano, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.

30Akaweka birika la kunawia katikati ya hema la mukutano na mazabahu, na kutia maji ya kunawa.

31Musa, Haruni na wana wake, wote wakanawa mikono na miguu yao mule.

32Kila mara walipoingia ndani ya hema au walipokaribia ile mazabahu, walinawa, kama vile Musa alivyoamuriwa na Yawe.

33Kwa mwisho Musa akatengeneza upango kuzunguka hema takatifu na mazabahu na kuweka pazia kwenye mulango wa upango. Hivyo, Musa akakamilisha kazi yote.

Wingu juu ya hema la mukutano(Hes 9.15-23)

34Kisha, lile wingu likafunika lile hema la mukutano na utukufu wa Yawe ukajaza hema.

35Musa akashindwa kuingia ndani ya hema la mukutano kwa sababu hilo wingu lilikaa juu yake na utukufu wa Yawe ukajaa mule.

36Katika safari zao zote Waisraeli hawakuanza safari hata kidogo isipokuwa wakati wingu hilo lilipoinuliwa kutoka juu ya hema.

37Kama wingu hilo halikuinuliwa wao hawakuanza safari. Walingoja mpaka wakati lilipoinuliwa.

38Katika safari zao zote, Waisraeli waliweza kuliona lile wingu la Yawe juu ya hema wakati wa muchana na ule moto ukiwaka juu yake usiku.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help