1Fikiri mbele ya kusema, wala usikuwe mwepesi kwa kusema neno lolote mbele ya Mungu, kwa maana Mungu yuko mbinguni na wewe uko katika dunia. Kwa hiyo usiseme maneno mengi.
2Kadiri mutu anavyohangaika zaidi, ndivyo atakavyoota ndoto;
sauti ya mupumbafu ni maneno mengi.
3Ukimutolea Mungu ahadi, usikawie kuitimiza. Mungu hapendezwi na wapumbafu. Timiza kile ulichoahidi.
4Ni afazali usifanye ahadi kuliko kufanya ahadi kisha usiitimize.
5Angalia kinywa chako kisikuingize katika zambi, halafu ikupase kumwambia mujumbe wa Mungu kwamba haukukusudia kutenda zambi. Kwa nini kumusukuma Mungu akukasirikie na kuiharibu kazi yako?
6Ndoto zikizidi, kuna maangamizi na maneno yanakuwa mengi. Jambo la maana ni kumwogopa Mungu.
Maisha ni bure7Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.
8Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.
9Yule anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayetamani mali hata akiipata hatatosheka. Hayo nayo ni bure.
10Mali ikiongezeka, wale watakaoikula wanaongezeka vilevile, naye mwenye mali inamufalia nini isipokuwa kuiangalia tu mali yake?
11Usingizi wa mutumishi ni mutamu, akuwe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi siku zote, maana mali yake inamuzuia kupata usingizi.
12Tena, nimeona jambo moja ovu sana chini ya jua: mutu alijikusanyia mali, ikakuwa hatari kwake.
13Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.
14Kama vile mwanadamu alivyokuja katika dunia akiwa uchi toka katika tumbo la mama yake, ndivyo atakavyorudi uchi kule alikotoka. Hataweza kupeleka hata sehemu ndogo ya mapato ya kazi yake.
15Hili nalo ni jambo baya sana. Atarudi kama vile alivyokuja. Amepata faida gani? Ametoa jasho kwa kukamata upepo.
16Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.
17Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.
18Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
19Na kwa kuwa Mungu amemuruhusu kuwa na furaha, mwanadamu hatakuwa na wasiwasi mwingi juu ya maisha yake mafupi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.