1Haleluia!
Mumwimbie Yawe wimbo mupya;
mumusifu katika kusanyiko la waaminifu!
2Umufurahie Muumba wako, ee Israeli;
ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.
3Mulisifu jina lake mukicheza,
mumwimbie kwa ngoma na zeze.
4Maana Yawe anapendezwa na watu wake;
yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.
5Waaminifu wafurahi, wakitukuza Mungu,
hata wanapolala.
6Wamusifu Mungu kwa sauti kubwa,
wakishika panga zenye kukata pande mbili,
7wawalipize mataifa kisasi,
wawaazibu watu;
8wawafunge wafalme wao kwa minyororo,
nao waongozi wao kwa vifungio vya chuma,
9kusudi wawaazibu sawa ilivyoamuriwa!
Na huu ndio utukufu wa waaminifu wa Mungu.
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.