Zaburi 6 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombi wakati wa taabu

1Kutoka Mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.

2Ee Yawe,

usiniazibu kwa hasira yako,

usiniadibishe kwa kasirani yako.

3Unihurumie, ee Yawe, nimeishiwa nguvu;

uniponyeshe, ee Yawe, ninatetemeka mpaka katika mifupa.

4Ninahangaika sana ndani ya roho yangu.

Ee Yawe, utakawia mpaka wakati gani?

5Unigeukie, ee Yawe, uniokoe;

uniponyeshe kwa sababu ya wema wako.

6Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka;

katika kuzimu ni nani anayeweza kukusifu?

7Ninatabanika kwa kulia kwa uchungu;

usiku ninalowanisha kitanda changu kwa machozi;

kwa kulia kwangu ninalowanisha matandiko yangu.

8Macho yangu yamechoka kwa huzuni;

yamefifia kwa kutaabishwa na waadui.

9Muondoke karibu nami, enyi wote watenda maovu!

Maana Yawe amesikia kilio changu.

10Yawe amesikia ombi langu;

Yawe amekubali maombi yangu.

11Waadui zangu wote watafezeheka na kufazaika;

watarudi nyuma na kufezeheka kwa rafla.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help