1Mufalme Solomono alitengeneza birika la maji la muviringo lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano na upana sawa na metre kenda, na urefu wake kwenda juu metre ine na nusu. Ang. Kut 27.1-2
2Kisha, akatengeneza birika la maji la muviringo, lenye upana wa metre ine na nusu kutoka ukingo mpaka ukingo, lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na lenye muzunguko wa metre kumi na tatu na nusu.
3Chini ya ukingo wake, kuzunguka lile birika, kulikuwa mistari miwili ya sanamu za ngombe dume, kwa metre kumi na tatu na nusu. Sanamu hizo za ngombe dume zilikuwa zimetengenezwa na shaba ileile wakati birika lilipofanywa.
4Nalo birika lilikuwa limewekwa juu ya sanamu za ngombe dume kumi na wawili, tatu zikielekea upande wa kaskazini, tatu upande wa magaribi, tatu kusini na zingine tatu upande wa mashariki.
5Unene wa ukingo wake ulikuwa sentimetre saba na nusu. Ukingo wake ulikuwa kama ukingo wa kikombe, na kama maua ya yungiyungi. Ndani ya birika lile kuliweza kuingia kadiri ya litre elfu makumi sita za maji.
6Akatengeneza vilevile beseni kumi za kusafishia sehemu za nyama zilizotumika katika sadaka za kuteketezwa kwa moto. Tano kati ya bakuli zile akaziweka upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Birika lilitumiwa na makuhani kwa kunawia. Ang. Kut 30.17-21
7Alitengeneza vinara kumi vya zahabu kama vile ilivyoagizwa, akaviweka katika baraza ya hekalu; vitano upande wa kusini, na vitano upande wa kaskazini. Ang. Kut 25.31-40
8Akatengeneza vilevile meza kumi, nazo akaziweka ndani ya chumba cha hekalu. Kisha akatengeneza beseni mia moja za zahabu. Ang. Kut 25.23-30
9Akatengeneza kiwanja cha ndani cha makuhani na kingine kikubwa cha inje, na milango ya kiwanja ambayo aliifunika na shaba;
10na lile birika akaliweka kwenye pembe ya kusini-mashariki ya nyumba.
11Hiramu akatengeneza vyungu, vipao na mabeseni. Basi Hiramu akamaliza kazi aliyomufanyia mufalme Solomono juu ya nyumba ya Mungu;
12nguzo mbili, mabakuli, taji mbili juu ya nguzo, na nyavu mbili kwa ajili ya kufunika mabakuli ya taji zilizowekwa juu ya nguzo;
13vilevile mifano ya makomamanga mia ine kwa ajili ya nyavu zile mbili, mistari miwili miwili ya makomamanga kwa kila wavu, kwa kupamba mabakuli yale mawili ya taji zilizokuwa juu ya kila nguzo.
14Vilevile akatengeneza beseni juu ya magari,
15na birika lile moja, na sanamu za ngombe dume kumi na wawili chini ya birika lile.
16Halafu vyungu, vipao na kanya na vyombo vingine vyote vya nyumba ya Yawe ambavyo Huruma-Abi alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.
17Vitu hivyo vyote mufalme alivitengeneza katika kiwanja cha Yordani, sehemu ya udongo wa mufinyanzi iliyokuwa kati ya Sukoti na Sereda.
18Uzito wa shaba iliyotumiwa kwa kutengeneza vyombo hivi haukujulikana kwa maana Solomono alitengeneza vyombo vingi sana.
19Solomono alitengeneza vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu: mazabahu ya zahabu na meza za mikate mitakatifu;
20vinara na taa za zahabu safi za kuangazia Pahali pale Patakatifu Sana, kama vile walivyoamuriwa;
21maua, taa na koleo, vyote vikiwa vya zahabu safi kabisa;
22makasi na mabeseni, sahani za kuwekea ubani na vyetezo vya kubebea moto, vyote vya zahabu safi, pete za hekalu za milango ya Pahali Patakatifu Sana, na za milango mingine ya vyumba vya ndani, zote zilitengenezwa na zahabu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.