Mezali 16 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Mwanadamu anapanga mipango yake, lakini neno la mwisho ni la Yawe.

2Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.

3Tegemea Yawe katika kazi yako, nayo mipango yako itafanikiwa.

4Yawe ameumba kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.

5Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Yawe. Hakika mutu wa namna hiyo hatakosa kuazibiwa.

6Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.

7Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.

8Afazali mali kidogo kwa njia ya haki, kuliko mapato mengi kwa njia isiyofuatana na sheria ya Mungu.

9Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.

10Mufalme anaamua kwa maongozi toka kwa Mungu. Anapotoa hukumu hapotoki.

11Mizani na vipimo vya kweli ni vya Yawe. Mawe yote ya kupimia katika mufuko ni kazi yake.

12Ni chukizo kubwa kwa wafalme kutenda uovu, maana musingi wa mamlaka yao ni haki.

13Mufalme anapendelea mutu anayesema maneno ya haki. Anamupenda mutu anayesema kwa usawa.

14Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.

15Uso wa mufalme ukiangaa, kuna uzima; kupendwa naye ni kama wingu la mvua kwa shamba.

16Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.

17Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.

18Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.

19Afazali kuwa munyenyekevu pamoja na masikini, kuliko kugawanyana vitu vya unyanganyi pamoja na wenye kiburi.

20Anayefikiri sana juu ya neno atafanikiwa. Heri mutu yule anayemutumainia Yawe.

21Mwenye hekima ndani ya moyo anaitwa mwenye akili; neno la kupendeza linawavuta watu.

22Hekima ni chemichemi ya uzima kwa yule anayekuwa nayo, lakini upumbafu ni azabu ya wapumbafu.

23Moyo wa mwenye hekima unamwezesha kusema kwa hekima; unayafanya maneno yake yakuwe ya kuvutia.

24Maneno mazuri ni kama asali. Ni matamu kwa nafsi na yenye kuupatia mwili afya.

25Kuna njia mutu anayoona kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.

26Njaa inamusukuma mutu kufanya kazi, maana tamaa ya kinywa chake inamupa bidii.

27Mutu mwovu anapanga kutenda uovu. Maneno yake ni kama moto mukali.

28Mutu mupotovu anatawanya ugomvi, na muchonganishi anatenganisha warafiki.

29Mutesaji mukali anamushawishi jirani yake na kumwongoza katika njia mbaya.

30Anayekonyeza jicho amepanga kutenda maovu; anayekaza midomo amekwisha kutenda mabaya.

31Kuwa na imvi za uzee ni taji la utukufu; zinapatikana kwa maisha ya haki.

32Asiyekuwa mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu. Anayetawala nafsi yake ni bora kuliko anayetaka muji.

33Kura inapigwa kwa kujua yatakayotukia, lakini uamuzi ni wa Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help