1Katika kabila la Benjamina, kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyeitwa Kisi. Yeye alikuwa mwana wa Abieli, mujukuu wa Zerori, wa jamaa ya Bekorati mwana wa Afia wa kabila la Benjamina.
2Kisi alikuwa na mwana aliyeitwa Saulo. Saulo alikuwa kijana mwenye sura nzuri, na hakuna mutu katika Israeli aliyelingana na Saulo kwa uzuri. Saulo alikuwa murefu zaidi kuliko mutu yeyote katika inchi ya Israeli; watu wote walimufikia kwenye mabega.
3Siku moja, punda wa Kisi, baba ya Saulo, walipotea. Hivyo, Kisi akamwambia Saulo: “Ukamate mutumishi mumoja, uende kuwatafuta punda.”
4Wakawatafuta kwenye inchi ya milima ya Efuraimu na eneo la Shalisa, lakini hawakuwaona kule. Halafu wakafika Salimu, na kule hawakuwaona. Wakawatafuta katika inchi ya Benjamina, hata hivyo hawakuwapata.
5Walipofika kwenye inchi ya Zufu, Saulo alimwambia mutumishi wake: “Turudie kwetu. Kama si vile, baba yangu ataacha kufikiri juu ya punda na kuwa na wasiwasi juu yetu.”
6Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”
7Saulo akamwuliza: “Lakini tukimwendea, tutamupa nini? Angalia, mikate katika mifuko yetu imekwisha na hatuna chochote cha kumupa yule mutu wa Mungu. Tuna nini?”
8Yule mutumishi akamujibu Saulo: “Ona, mimi nina vikoroti vine vya shekeli. Nitamupa huyo mutu wa Mungu kusudi atuambie juu ya safari yetu.”
9(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).
10Saulo akamujibu: “Hilo ni jambo zuri; basi, tuende.”
Hivyo, wakaenda kwenye muji mutu yule wa Mungu alimokuwa anakaa.
11Walipokuwa wanapanda mulima kuelekea katika muji, wakakutana na wabinti waliokuwa wakienda kuteka maji. Wakawauliza wabinti wale: “Mwonaji yuko katika muji?”
12Wale wabinti wakawajibu: “Ndiyo, yuko. Tena yuko mbele yenu; mukifanya haraka mutamukuta. Ameingia katika muji leo tu, kwa sababu leo watu watatoa sadaka kule kwenye mulima.
13Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”
14Hivyo Saulo na mutumishi wake walikwenda katika muji. Walipokuwa wanaingia katika muji, walimwona Samweli akitoka katika muji, na anaelekea kwenda kwenye nafasi ya kuabudia.
15Jana yake, mbele ya Saulo kufika katika muji pale, Yawe alikuwa amemwambia Samweli hivi:
16“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”
17Samweli alipomwona tu Saulo, Yawe alimwambia: “Huyu ndiye mutu yule niliyekuambia. Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
18Hapo Saulo alimwendea Samweli aliyekuwa karibu na mulango wa muji na kumwuliza: “Ninakuomba unionyeshe nyumba ya mwonaji.”
19Samweli akamujibu: “Mimi ndiye mwonaji. Munitangulie kwenda kwenye nafasi ya kuabudia maana leo mutakula pamoja nami. Kesho asubui maulizo yote unayokuwa nayo nitayajibu.
20Na juu ya wale punda waliopotea siku tatu zilizopita, musikuwe na wasiwasi juu yao; wamekwisha kupatikana. Lakini ni nani yule ambaye Waisraeli wanamutaka sana? Si wewe na jamaa yote ya baba yako?”
21Saulo akajibu: “Mimi ni wa kabila la Benjamina, kabila dogo kuliko makabila yote ya Waisraeli. Na katika kabila lote la Benjamina jamaa yangu ndiyo ndogo kabisa. Lakini, kwa nini unanizungumuzia namna hiyo?”
22Kisha Samweli akamupeleka Saulo na mutumishi wake ndani ya baraza, akawapa nafasi ya heshima, ambako wageni walioalikwa walikuwa wameikaa. Kulikuwa wageni yapata makumi tatu.
23Samweli akamwambia mupishi: “Ulete ile sehemu niliyokupatia, nikakuambia uiweke pembeni.”
24Yule mupishi akaenda akaleta paja na sehemu ya nyama iliyokuwa upande wa juu wa paja hilo na kuviweka mbele ya Saulo. Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Angalia kile ulichowekewa; sasa kimewekwa mbele yako. Sasa ukule kwa sababu kimewekwa kwa ajili yako kusudi upate kula pamoja na wageni.”
Hivyo, Saulo akakula pamoja na Samweli siku hiyo.
25Waliporudi katika muji kutoka kwenye nafasi ya ibada juu ya mulima, alizungumuza na Saulo juu ya dari. Na Saulo akalala kule.
Samweli anamupakaa Saulo mafuta26Kesho yake asubui mapema, Samweli alimwita Saulo kutoka juu ya dari: “Amuka, kusudi nikusindikize urudi kwa nyumba.” Saulo aliamuka, na wote wawili, yeye na Samweli, wakatoka na kwenda katika barabara.
27Walipofika mwisho wa muji, Samweli akamwambia Saulo: “Umwambie yule kijana atangulie mbele yetu.” Kijana alipokwisha ondoka, Samweli akaendelea kusema: “Ngoja kidogo, nami nitakufunulia yale Mungu aliyosema.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.