1Zaburi ya Wakora: Wimbo.
Mungu amejenga muji wake
juu ya mulima wake mutakatifu.
2Yawe anapenda Sayuni,
kuliko makao mengine ya Yakobo.
3Ee muji wa Mungu,
mambo ya utukufu yanasemwa juu yako.
4Kati ya wale wanaonijua mimi,
kuna Wamisri na Wababeli.
Vilevile Wafilistini, Watiro na Waetiopia.
Wanasema: “Huyu amezaliwa kule.”
5Lakini juu ya Sayuni itasemwa:
“Sayuni ni mama yao wote;
Mungu Mukubwa atauimarisha.”
6Yawe atakapohesabu watu,
ataandika hivi katika kitabu:
“Huyu amezaliwa kule!”
7Wote wanacheza ngoma na kuimba:
“Sayuni shina letu ni kwako.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.