Ezekieli UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKatika mwaka wa 597 mbele ya Kristo, nabii Ezekieli pamoja na mufalme Yoyakinu na watu wenye sifa wa Yerusalema, walipelekwa katika uhamisho katika inchi ya Babeli. Ezekieli alitoa mahubiri yake akiwa huko. Yaliwaelekea hao watu waliohamishwa na wale waliobaki Yerusalema.Kitabu cha Ezekieli kina sehemu ine:Sura 1-24. Maonyo kwa watu juu ya hukumu ya Yawe inayokuja. Hukumu hiyo inaelekea kuangamizwa kabisa kwa inchi ya Yuda na Yerusalema.Sura 25-32. Sehemu hii inaonyesha wazi kwamba hukumu ya Mungu itawapata vilevile watu wa mataifa mengine ambao waliwatendea vibaya na kuwauzi Waisraeli.Sura 33-39. Sehemu hii kwa jumla ina maneno ya matumaini kwa kuwatia moyo Waisraeli kisha hasara ya kutekwa kwa Yerusalema.Sura 40-48 Maonyo ya Ezekieli juu ya hekalu mupya na matengano ya watu wa Mungu.