Zefania UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIZefania alihubiri ujumbe wa Mungu katika inchi ya Yuda kati ya mwaka wa 640 na 620 mbele ya Kristo.Kitu kikubwa katika mahubiri yake ni kwamba Mungu atawaazibu watu wa Yuda na Yerusalema kwa sababu walitumikia miungu ya uongo. Wakati huo atakapowaazibu ndio wakati ule unaotajwa kama Siku ya Yawe. Hata mataifa jirani na Yuda nayo vilevile yataazibiwa. Lakini katika siku zinazokuja Yerusalema itamutumikia Mungu, naye Mungu atawafanikisha tena watu wake.