1Sasa tunawaandikia juu ya mambo yanayoelekea kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo na namna sisi tutakavyokusanyika mbele yake. Wandugu, tunawasihi sana,
2musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.
3Musikubali kudanganywa na mutu yeyote kwa namna yoyote. Kwa maana Siku ile haitatimia mpaka kwanza ule uasi mukubwa utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa.
4Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.
5Hamukumbuki kwamba niliwaambia maneno haya wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
6Lakini munajua kitu kinachozuiza mambo haya kutokea sasa. Kwa hivi yule Mwovu atatokea kwa wakati wake uliopangwa.
7Hata hivi yule Mwovu anatenda kazi zake kwa siri; lakini yule anayezuiza ataendelea hata atakapoondoshwa.
8Halafu, yule Mwovu atatokea, lakini Bwana Yesu atakapotokea atamwua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa nguvu za kumetameta kwake.
9Mwovu atakuja na uwezo wa Shetani na kufanya miujiza ya kila namna, vitambulisho na maajabu ya uongo.
10Atatumia ubaya wa kila namna kwa kuwadanganya wale wanaopotea kwa sababu hawakupenda kukubali na kupenda mambo ya kweli yaliyoweza kuwaokoa.
11Kwa sababu hii Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu wapate kuamini mambo ya uongo.
12Kwa hivi wale wote wasioamini maneno ya ukweli, waliofurahia mambo mabaya watahukumiwa.
Kusimama imara katika imani13Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.
14Mungu amewaalika kuwa vile kwa njia ya Habari Njema tuliyowatangazia, kusudi mupate kushiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15Basi wandugu, musimame imara na mushike mafundisho yetu tuliyowatolea, ikiwa kwa mahubiri au kwa barua yetu.
16Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,
17awafariji na kuwaimarisha katika matendo na maneno yote mema.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.