Mezali 19 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Afazali masikini mwenye mwenendo mukamilifu kuliko mutu mupotovu wa maneno na mupumbafu.

2Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.

3Mutu akijiangamiza kwa upumbafu wake, anaielekeza hasira yake kwa Yawe.

4Mali inavuta warafiki wengi wapya, lakini masikini anaachwa na rafiki yake.

5Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo hataepuka azabu.

6Watu wengi wanajipendekeza kwa wakubwa; kila mutu anataka kuwa rafiki wa mutu mwenye kupana.

7Masikini anachukiwa na wandugu zake; warafiki zake ndio zaidi: wanamukimbia! Hata awabembeleze namna gani, hatawapata.

8Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.

9Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo ataangamia.

10Haifai kwa mupumbafu kuishi kwa raha; tena ni vibaya zaidi mutumwa kuwatawala wakubwa.

11Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.

12Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.

13Mutoto mupumbafu ni hasara kwa baba yake; na ugomvi wa muke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.

15Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.

16Anayeshika amri analinda maisha yake; anayezarau agizo atakufa.

17Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.

18Azibu mwana wako wakati kungali bado tumaini lakini usitafute kumwangamiza.

19Mutu wa hasira kali anapaswa kupata azabu; ukimwachilia mara moja itakuomba kumwachilia tena.

20Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.

21Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.

22Kitu kinachotakiwa kwa mutu ni uaminifu; afazali mutu masikini kuliko mutu mwongo.

23Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.

24Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.

25Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.

26Anayemutesa baba yake na kumufukuza mama yake ni mutoto asiyefaa na mupotovu.

27Mwana wangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, mara moja utapotea mbali na maneno ya maarifa.

28Mushuhuda asiyefaa kitu anazarau sheria ya Mungu; na kinywa cha mwovu kinameza uovu.

29Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help