2 Mambo ya Siku 31 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Matengenezo ya ibada

1Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.

2Mufalme Hezekia akawapanga tena makuhani na Walawi katika makundi, akamupa kila mumoja wao kazi kufuatana na utumishi wake katika sehemu mbalimbali za hekalu la Yawe. Kazi ile ni pamoja na utoaji wa sadaka za kuteketeza kwa moto na za amani, za shukrani na za kusifu.

3Kutoka mali yake mwenyewe, mufalme akatoa sehemu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa asubui na magaribi, za siku ya Sabato na wakati wa sherehe za mwandamo wa mwezi na zile sikukuu zingine zilizoamuriwa kulingana na Sheria ya Yawe. na zaidi, na ambao waliingia katika nyumba ya Yawe kila siku kwa kutimiza kazi zao. Kila mumoja wao alipata sehemu yake kulingana na kazi aliyofanya kwa zamu yake.

17Makuhani waliandikishwa kulingana na jamaa zao, na Walawi waliotimiza miaka makumi mbili na zaidi waliandikishwa kulingana na kazi zao na zamu zao.

18Waliandikishwa wote pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, wana wao na wabinti zao kwa sababu, kwa kujitoa kwa kazi zao, walihitajika kujiweka katika hali ya utakaso kila mara.

19Vilevile, kati ya wazao wa Haruni, makuhani waliokuwa wanakaa katika mashamba waliyorizi kwa pamoja inje ya miji yao, kulikuwa watu waliochaguliwa kwenye miji hiyo ambao waliwagawanyia sehemu zao za vyakula. Waliwapa sehemu kila mwanaume katika jamaa za makuhani, na kila mumoja aliyekuwa ameandikishwa kati ya Walawi.

20Hivi ndivyo mufalme Hezekia alivyotenda mambo mema, ya haki na ya uaminifu mbele ya Yawe, Mungu wake, katika inchi yote ya Yuda.

21Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help