1Enyi watu wa kabila la Benjamina,
muondoke Yerusalema, mukimbie!
Mupige baragumu katika muji Tekoa!
Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu,
maana hasara na maangamizi makubwa
vinakuja kutoka upande wa kaskazini.
2Muji wa Sayuni ni muzuri na wenye kupendeza,
lakini utaharibiwa.
3Watu wataufikia kama vile wachungaji na makundi yao,
watasimamisha hema zao kandokando yake,
kila wamoja upande wao kwa kulisha makundi yao.
4Halafu watasema: Mujitayarishe, tupigane vita na Sayuni.
Musimame, tuushambulie pa saa sita za muchana!
Bahati mbaya kwetu, maana jua linatua!
Saa za magaribi zinakaribia.
5Basi, tutaushambulia usiku;
tutaziharibu nyumba zake nzuri zote.
6Yawe wa majeshi anasema hivi:
Mukate miti na kulundika udongo,
kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema.
Muji huu unapaswa uazibiwe,
maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.
7Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima,
ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema.
Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake.
Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.
8Basi usikilize maonyo, ee Yerusalema.
Kama sivyo nitakutupilia mbali;
nitakufanya ukuwe jangwa,
kuwa pahali pasipokaliwa na mutu.
Watu wasiopenda kusikia9Yawe wa majeshi anasema hivi:
Muwakusanye watu wote wa Israeli waliobaki
kama vile watu wanavyookotesha zabibu katika shamba;
kama vile muchumaji wa zabibu,
mupitishe mikono katikati ya matawi yote.
10Nitaongea na nani nipate kumwonya,
kusudi wapate kunisikia?
Angalia, masikio yao yameziba,
hawawezi kusikia ujumbe wako.
Maneno ya Yawe,
yamegeuka kwao jambo la kuchekelea.
Hawalifurahii hata kidogo.
11Nimejaa hasira ya Yawe
nami ninachoka kwa kuizuia.
Kwa hiyo Yawe akaniambia:
Umwange hasira ile katika barabara juu ya watoto
na vilevile juu ya makundi ya vijana;
nayo itawaangukia wote, mume na muke,
nao wazee na hata wale ambao wamezeeka sana.
12Nyumba zao zitapewa watu wengine,
nayo mashamba yao na wake zao vilevile;
maana nitaunyoosha mukono wangu,
kuwaazibu wakaaji wa inchi hii.
–Ni ujumbe wa Yawe.
13Wote, tangu mudogo mpaka mukubwa kabisa,
kila mumoja anatamani kupata faida isiyokuwa ya haki.
Tangu manabii mpaka makuhani,
kila mumoja wao ni mudanganyifu.
14Wanatunza vidonda vya watu wangu juujuu,
wakisema: “Kuna amani, kuna amani”,
ingawa hakuna amani yoyote!
15Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo?
Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo.
Hata zamiri hazikuwagonga.
Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka;
wakati nitakapowaazibu,
wataangamizwa kabisa.
–Ni Yawe anayesema hivyo.
Israeli anakataa njia ya Mungu16Yawe anasema hivi:
Musimame katika masanganjia, muangalie.
Muulize juu ya matukio ya zamani.
Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri
muifuate, nanyi mutaweza kupumzika.
Lakini wao wakasema:
Hatutafuata njia hiyo.
17Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia:
Musikilize mulio wa baragamu.
Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.
18Kwa hiyo, musikilize, enyi mataifa;
enyi makundi ya watu, mujue yale yatakayowapata.
19Sikiliza, ee dunia!
Mimi nitawaletea watu hawa hasara
kulingana na nia zao mbaya.
Maana hawakuyajali maneno yangu,
na mafundisho yangu nayo wameyakataa.
20Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba,
na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali?
Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki,
wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.
21Kwa hiyo Yawe anasema hivi:
Nitawawekea watu hawa vikwazo,
ambavyo vitawaangusha chini.
Wababa na wana wataangamia,
na jirani na rafiki vilevile.
Mashambulizi kutoka kaskazini22Yawe anasema hivi:
Muangalie, watu wanakuja toka inchi ya kaskazini;
taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali kwa mwisho wa dunia.
23Wameshika pinde zao na mikuki;
ni watu wakali wasiokuwa na huruma.
Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari.
Wamepanda juu ya farasi,
wamejipanga tayari kwa vita
na wewe Sayuni!
24Waisraeli wanasema:
Tumesikia habari zao.
Kwa hiyo mikono yetu imeregea;
tumeshikwa na huzuni na uchungu,
kama mwanamuke anayezaa.
25Hatuwezi kwenda katika mashamba,
wala kutembea katika barabara;
waadui wameshika silaha katika mikono,
vitisho vimejaa kila pahali.
26Yawe anasema:
Muvae magunia, enyi watu wangu
na kugaagaa katika majivu.
Muomboleze kwa uchungu,
kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee,
maana mwangamizaji atakuja,
na kuwashambulia kwa rafla.
27Yeremia, wewe nimekuweka kuwa muchunguzi
na mupimaji wa watu wangu,
kusudi uchunguze na kuzijua njia zao.
28Wote ni waasi na wagumu,
ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine,
ni wagumu kama shaba au chuma.
Wote wanatenda mabaya.
29Moto wa kufua vyuma unawaka kwa nguvu,
risasi inayeyukia humohumo katika moto;
ni bure kuendelea kuwatakasa watu wangu,
waovu hawawezi kuondolewa uchafu wao.
30Basi wataitwa “takataka za feza”,
maana mimi Yawe nimewakataa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.