Waamuzi 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Yawe aliyaacha kwa kuwajaribu Waisraeli ambao walikuwa hawajapigana vita katika inchi ya Kanana.

2Alifanya hivyo kusudi awape watu wa vizazi hivyo ujuzi wa kupigana maana hawakukuwa wameona vita.

3Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.

4Yawe alikusudia kuwatumia hao kusudi awajaribu Waisraeli, aone kama watatii amri zake alizowaamuru wazee wao kwa njia ya Musa.

5Basi, Waisraeli waliishi pamoja na Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

6Wakaoa wabinti zao na kuoesha wabinti zao kwa vijana wa mataifa hayo na kuiabudu miungu yao.

Otinieli

7Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe. Wakamusahau Yawe, Mungu wao, wakaabudu Mabali na Maashera.

8Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya mufalme wa Mesopotamia, jina lake Kusani, Yule-Mwovu-Sana. Wakamutumikia kwa muda wa miaka minane.

9Waisraeli wakamulilia Yawe, naye akawapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu mudogo wa Kalebu.

10Basi, roho wa Yawe akamujaza Otinieli, naye akakuwa mwamuzi wa Waisraeli. Otinieli alikwenda katika vita naye Yawe akamutia Kusani, Yule-Mwovu-Sana, ufalme wa Mesopotamia, katika mikono yake.

11Inchi ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine. Kisha Otinieli mwana wa Kenazi, akakufa.

Ehudu

12Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe. Yawe akamutia nguvu mufalme wa Moabu aliyeitwa Mwana-Ngombe kusudi awashambulie Waisraeli, kwa sababu walitenda uovu mbele ya Yawe.

13Mufalme Mwana-Ngombe akawakusanya Waamori na Waamaleki, akaenda kupigana na Waisraeli, akawashinda. Akauteka Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema Yeriko.

14Waisraeli wakamutumikia Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu, kwa muda wa miaka kumi na minane.

15Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto.

Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.

16Ehudu akajitengenezea upanga wenye makali ngambo mbili; urefu wake sentimetre makumi tano. Akaufunga kwenye kiuno chake upande wa kuume ndani ya nguo yake.

17Kisha akamupelekea Mwana-Ngombe zile zawadi. Mwana-Ngombe alikuwa mutu munene sana.

18Ehudu alipomaliza kutoa zawadi, akawaambia watu waliobeba zawadi waondoke.

19Lakini yeye alipofika kwenye sanamu za mawe yaliyochongwa karibu na Gilgali, akamurudilia Mwana-Ngombe akasema: “Nina ujumbe wa siri kwako, ee mufalme.” Mufalme akawaamuru watumishi wakae kimya, nao wakatoka inje.

20Naye Ehudu akamukaribia pale alipokaa katika chumba chake chenye baridi katika baraza, akamwambia: “Nina ujumbe wako kutoka kwa Mungu.” Mufalme akasimama toka juu ya kiti chake.

21Ehudu akauchomoa upanga wake kwa mukono wake wa kushoto kutoka paja lake la kuume, akamuchoma nao katika tumbo lake.

22Upanga ukaingia ndani pamoja na mupini wake, mafuta yakaufunika upanga ule maana Ehudu hakuutoa tena; ukakuwa umetokea kwa nyuma.

23Kisha, Ehudu akatoka inje ndani ya baraza kisha kuifunga milango ya chumba hicho kwa ufunguo.

24Ehudu alipoondoka, watumishi wa mufalme wakarudi. Walipoona milango yote ya chumba imefungwa, wakafikiri kwamba amekwenda kujisaidia kwenye choo mule ndani ya nyumba.

25Wakangojea mpaka wakaanza kuona wasiwasi. Walipoona hafungui, wakatwaa ufunguo na kufungua mulango. Wakamwona mufalme wao chini, naye amekufa.

26Walipokuwa wanangoja, Ehudu akatoroka akipitia kwenye sanamu za mawe, akaenda Seira.

27Alipofika kule akapiga baragumu katika inchi ya milima ya Efuraimu, nao Waisraeli wakateremuka pamoja naye kutoka kule kwenye milima naye akawatangulia.

28Akawaambia: “Munifuate, maana Yawe amewatia waadui zenu Wamoabu katika mikono yenu.” Wakamufuata mpaka kwenye kivuko cha Yordani na kukiteka toka katika mikono ya Wamoabu, wakazuia mutu yeyote kupita.

29Siku hiyo, wakawaua Wamoabu yapata elfu kumi, wote wenye afya na nguvu, wala hakuna hata mumoja aliyeponyoka.

30Siku hiyo Waisraeli wakawashinda Wamoabu. Inchi ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi nane.

Samugari

31Nyuma ya Ehudu mwana wa Anati, Samugari akakamata nafasi yake. Yeye aliwaua Wafilistini mia sita kwa fimbo ya kuchunga ngombe. Naye vilevile aliwakomboa Waisraeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help