1Basi hawa watu watatu: Elifasi, Bildadi na Zofari, wakaacha kumujibu Yobu kwa vile alijiona kuwa mwenye haki.
2Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi wa ukoo wa Rama akakasirika. Alimukasirikia Yobu kwa sababu Yobu alijiona yeye mwenye haki na wala si Mungu.
3Vilevile, aliwakasirikia warafiki watatu wa Yobu kwa sababu hawakukuwa na neno la kumujibu Yobu, na kwa hiyo wakaonyesha kwamba Mungu amekosa.
4Elihu alikuwa amekaa kimya wakati wale wazee waliposema na Yobu kwa maana yeye alikuwa kijana kuliko wao.
5Lakini alipoona wale watu watatu wameshindwa kumujibu Yobu, akawaka hasira.
6Basi, Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi, akaanza kusema:
Mimi ni kijana, ninyi ni wazee zaidi.
Kwa hiyo niliogopa kuwaambia mawazo yangu.
7Nilisema ndani ya moyo: “Uwaache wenye siku nyingi waseme,
wenye miaka mingi wafundishe hekima.”
8Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu,
ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo,
ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.
9Si lazima kuwa muzee kusudi ukuwe na hekima;
haiko wazee tu ndio wenye kufahamu jambo linalokuwa sawa.
10Kwa hiyo ninasema: “Munisikilize,
muache nami nitoe maoni yangu.”
11Basi, mimi nilingojea kile mulichotaka kusema,
nilisikiliza misemo yenu ya hekima,
mulipokuwa munajaribu kutafuta neno la kusema.
12Niliwasikiliza kwa uangalifu sana,
lakini hakuna hata mumoja wenu aliyemushinda Yobu;
wote mulishindwa kujibu kwa maneno yake.
13Kwa hiyo musiseme: “Sasa tumepata hekima.
Atakayemushinda ni Mungu, wala si mwanadamu.”
14Maneno ya Yobu hayakukuwa kwa ajili yangu.
Kwa hiyo sitamujibu kama vile mulivyomujibu ninyi.
15Ninyi mumeshangaa na kukaa kimya;
ninyi hamuna cha kusema zaidi.
16Basi, ningoje tu kwa vile hamusemi,
kwa sababu munakaa tu bila kujibu kitu?
17Mimi vilevile nitatoa jibu langu;
mimi nitatoa vilevile maoni yangu.
18Niko na maneno mengi sana,
roho yangu inanisukuma kusema.
19Moyo wangu umefurika kama divai iliyozibwa,
kama kibuyu cha divai mupya tayari kupasuka.
20Ni lazima niseme kusudi nipate kutulia;
inanipasa kufungua kinywa changu na kujibu.
21Sitamupendelea mutu yeyote
wala kutumia maneno ya kubembeleza mutu,
22maana mimi sijui kubembeleza mutu.
Kama si vile, Muumba wangu angeniangamiza.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.