1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo. Mimi niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa Efeso, munaokuwa waaminifu katika kuungana na Yesu Kristo.
2Ninawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Baraka tunazopewa kwa njia ya Kristo3Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.
4Mbele ya kuumbwa kwa dunia, Mungu alituchagua kuwa watu wake kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watakatifu na pasipo kilema mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5Mungu amekusudia tangu zamani kutukubali sisi kuwa watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Alifanya vile kufuatana na mapenzi yake.
6Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.
7Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake
8akitupatia hekima na akili kamili.
9Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.
10Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.
11Mungu amefanya kila kitu kufuatana na kusudi na mapenzi yake. Yeye ametuchagua kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watu wake.
12Kwa hiyo sisi tuliotangulia kumutumainia Kristo, tumusifu Mungu kwa ajili ya utukufu wake!
13Ninyi vilevile, wakati muliposikia ujumbe wa kweli, maana yake Habari Njema iliyowaletea wokovu, mukamwamini Kristo. Naye Mungu akawapatia Roho Mutakatifu aliyeahidi kuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba ninyi ni watu wake kabisa.
14Yule Roho ni rehani ya urizi aliowawekea watu wake. Na jambo hili linahakikisha kwamba Mungu atakomboa kabisa wote wanaokuwa wake. Tumusifu kwa ajili ya utukufu wake.
Maombi ya Paulo15Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia namna munavyomwamini Bwana Yesu na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu,
16mimi sichoki kumushukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika maombi yangu.
17Ninamwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye utukufu, awapatie Roho wake kusudi mukuwe na hekima na ufunuo hata muweze kumujua.
18Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,
19na kutambua jinsi uwezo wake unavyokuwa mukubwa sana kwa ajili yetu sisi waamini, akizitumia nguvu zake kubwa sana.
20Alifanya vile wakati alipomufufua Kristo na kumwikalisha na mamlaka kwa kuume kwake mbinguni.
21Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.
22Mungu amemupatia Kristo mamlaka juu ya vitu vyote na kumuweka kuwa kichwa cha kanisa.
23Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.