Yoshua 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Eneo lililokuwa bado kutwaliwa

1Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.

2Sehemu hizo ni: inchi yote ya Wafilistini na inchi yote ya Wagesuri,

3ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,

4upande wa kusini. Vilevile inchi za Wakanana kuanzia Ara ya Wasidoni mpaka Afeki kwa mupaka wa Waamori;

5vilevile eneo la Gebali na Lebanoni upande wa mashariki ya Bali-Gadi chini ya mulima Hermoni mpaka Lebo-Hamati;

6vilevile eneo la milima inayokuwa kati ya Lebanoni na Misirepoti-Maimu ambayo wakaaji wake ni Wasidoni. Kadiri na jinsi Waisraeli watakavyoendelea mbele, mimi mwenyewe nitayafukuza mataifa hayo katika inchi hizo mbele yao. Nawe utawagawanyia Waisraeli sehemu mbalimbali za inchi hizo kwa kura kama nilivyokuamuru.

15Sehemu ya inchi ambayo Musa aliwapa watu wa kabila la Rubeni kulingana na jamaa zao,

16ilikuwa kuanzia Aroeri pembeni ya bonde la Arnoni na muji uliokuwa katika bonde hilo pamoja na inchi yote ya bonde ya Medeba.

17Ilikuwa vilevile pamoja na Hesiboni na miji yake yote inayokuwa katika sehemu ya bonde: ni kusema Diboni, Bamoti-Bali, Beti-Bali-Meoni,

18Yasa, Kedemoti, Mefati,

19Kiriataimu, Sibuma, Zereti-Sahari, kule kwa kilima katika bonde,

20Beti-Peori, miteremuko ya mulima Pisiga, Beti-Yesimoti

21na miji yote ya mabonde, inchi yote ya mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alitawala kule Hesiboni; Musa alikuwa amemushinda huyu Sihoni pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, ambao walitawala inchi kwa jina la mufalme Sihoni.

22Balamu mwaguzi mwana wa Beori ambaye Waisraeli walimwua alikuwa mumoja wao.

23Mupaka wa inchi ya kabila la Rubeni upande wa magaribi ulikuwa muto Yordani. Miji na maeneo yaliyotajwa hapa ndiyo sehemu waliyopewa watu wa ukoo za kabila la Rubeni.

24Sehemu ya inchi ambayo Musa aliwapa watu wa kabila la Gadi kulingana na ukoo zao

25ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya inchi ya Waamoni mpaka Aroeri kwa upande wa mashariki wa Raba.

26Vilevile kuanzia Hesiboni mpaka Ramati-Misipe, Betonimu, na kutokea Mahanaimu hata kwa mupaka wa Debiri.

27Vilevile miji iliyokuwa katika bonde la Beti-Haramu, Beti-Nimura, Sukoti na Zafoni na inchi yote iliyokuwa ya mufalme Sihoni wa Hesiboni; eneo hilo lilikuwa upande wa mashariki wa Yordani na kupakana na upande wa kusini wa bahari ya Kineroti.

28Miji na vijiji hivi ndivyo watu wa kabila la Gadi walivyopewa kulingana na ukoo zao.

29Tena, Musa alikuwa ameipatia nusu ya kabila la Manase kulingana na ukoo zake,

30eneo la inchi kuanzia Mahanaimu mpaka kuingia katika inchi yote iliyokuwa ya mufalme Ogi katika Basani, pamoja na miji makumi sita ya Yairi,

31nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.

32Musa alikuwa amewagawanyia sehemu hizo mbalimbali za inchi iliyokuwa upande wa mashariki wa Yeriko na Yordani, wakati alipokuwa kwenye mabonde ya Moabu.

33Lakini kabila la Lawi, Musa hakulipa sehemu yao ya inchi, maana aliwaambia kwamba sehemu yao itakuwa kumutumikia Yawe, Mungu wa Israeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help