1Mufalme mumoja Mukanana wa Aradi aliyeishi kule Negebu alipopata habari kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atarimu, akakwenda kuwashambulia na kuwateka wamoja kati yao.
2Hapo, Waisraeli wakamwekea Yawe kiapo wakisema: Kama ukiwatia watu hawa katika mikono yetu, basi tutaangamiza kabisa miji yao.
3Yawe akasikia ombi lao, akawapa ushindi juu ya Wakanana. Waisraeli wakaangamiza kabisa Wakanana pamoja na miji yao. Kwa hiyo pahali pale pakaitwa Horma, ni kusema “Maangamizi”.
Nyoka wa shaba4Waisraeli wakafunga safari kutoka mulima Hori, wakapitia njia inayoelekea bahari Nyekundu kusudi wazunguke inchi ya Edomu. Lakini katika njia watu wakavunjika moyo.
5Basi, wakaanza kumunungunikia Mungu na Musa, wakisema: Kwa nini mumetutoa Misri tukuje tukufie humu katika jangwa? Humu hamuna chakula wala maji; nasi tumechokeshwa na chakula hiki cha bure.
6Hapo Yawe akatuma nyoka wenye sumu kati ya watu, wakawauma hata Waisraeli wengi wakakufa.
7Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.
8Halafu Yawe akamwambia Musa: Tengeneza nyoka wa shaba, umutundike juu ya muti. Mutu yeyote atakayeumwa na nyoka, akiangalia kwenye nyoka huyo wa shaba, atapona.
9Basi, Musa akatengeneza nyoka wa shaba, akamutundika juu ya muti. Kila mutu aliyeumwa na nyoka alipomuangalia nyoka huyo wa shaba, alipona.
Safari mpaka bonde la Wamoabu10Waisraeli wakaendelea na safari yao, wakapiga kambi kule Oboti.
11Kutoka kule wakasafiri mpaka Iye-Abarimu, katika jangwa upande wa mashariki wa Moabu.
12Kutoka kule wakasafiri wakapiga kambi yao katika bonde la Zeredi.
13Kutoka huko wakasafiri, wakapiga kambi upande wa kaskazini wa muto Arnoni, ambao unatiririka kutoka katika inchi ya Waamori na kupitia katika jangwa. Muto Arnoni ulikuwa mupaka kati ya Wamoabu na Waamori.
14Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita za Yawe: “Muji wa Wahebu katika inchi ya Sufa, na mabonde ya Arnoni,
15na muteremuko wa mabonde unaofika mpaka muji wa Ari, na kuelekea kwenye mupaka wa Moabu.”
16Kutoka huko Waisraeli wakasafiri mpaka Beri; ni kusema kisima ambapo Yawe alimwambia Musa: Uwakusanye watu pamoja, nami nitawapa maji.
17Hapo Waisraeli wakaimba wimbo huu:
Bubujika maji, ee kisima! Muimbe!
18Kisima kilichochimbwa na wakubwa
kilichochimbwa sana na wenye cheo,
kwa fimbo zao za utukufu na bakora.
Kutoka katika jangwa wakasafiri mpaka Matana,
19kutoka Matana mpaka Nahalieli, kutoka Nahalieli mpaka Bamoti,
20na kutoka Bamoti mpaka kwenye bonde linaloingia katika inchi ya Moabu, kwenye kilele cha mulima Pisiga, kinachoelekea chini katika jangwa.
Waisraeli wanashinda wafalme Sihoni na Ogi(Kumb 2.26–3.11)21Waisraeli wakamupelekea mufalme Sihoni wa Waamori, ujumbe huu:
22Uturuhusu tupite katika inchi yako; hatutakwenda pembeni na kuingia katika mashamba au katika mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visima vyenu; tutapita moja kwa moja katika barabara kubwa ya mufalme mpaka tutakapoondoka katika inchi yako.
23Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapite katika inchi yake. Akawakusanya watu wake, akaenda Yahasa katika jangwa kwa kuwashambulia Waisraeli.
24Lakini Waisraeli wakamwua kwa makali ya upanga, wakatwaa inchi yake, tangu muto Arnoni mpaka muto Yaboki, mpaka inchi ya Waamoni; nao mupaka wa inchi ya Amoni ulikuwa unalindwa sana.
25Waisraeli wakaiteka miji hii yote nao wakaishi katika miji ya Waamori katika Hesiboni na vijiji vyake.
26Hesiboni ulikuwa muji wa Sihoni mufalme wa Waamori, ambaye mbele alikuwa amepigana na mufalme wa Moabu na kuteka inchi yake yote mpaka muto Arnoni.
27Ndiyo maana washairi wetu wanaimba:
Mukuje Hesiboni na kujenga.
Muji wa Sihoni ujengwe na kuimarishwa.
28Maana moto ulitoka Hesiboni,
miali ya moto ilitoka katika muji kwa Sihoni,
ukauteketeza muji wa Ari wa Moabu,
ukaiangamiza milima ya muto Arnoni.
29Ole wenu watu wa Moabu!
Mumeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemosi!
Umewafanya watoto wenu wanaume kuwa wakimbizi,
wabinti zako umewaacha watwaliwe mateka
mpaka kwa Sihoni, mufalme wa Amori.
30Lakini sasa wazao wao wameangamizwa,
kutoka Hesiboni mpaka Diboni,
kutoka Nasimu mpaka Nofa, karibu na Medeba.
31Basi, Waisraeli wakakaa katika inchi ya Waamori.
32Kisha Musa akatuma watu wapeleleze muji wa Yazeri; wakauteka pamoja na vijiji vyake, wakawafukuza Waamori waliokaa humo.
33Waisraeli wakageuka wakafuata njia inayoenda Basani. Mufalme Ogi wa Basani akatoka na jeshi lake kwa kuwashambulia huko Edirei.
34Lakini Yawe akamwambia Musa: Usimwogope, maana nimemutia katika mikono yako pamoja na watu wake wote na inchi yake yote. Utamutendea kama ulivyomutendea Sihoni, mufalme wa Waamori, aliyekuwa anakaa Hesiboni.
35Basi, Waisraeli wakamwua Ogi, wana wake na watu wake wote, bila kumwacha hata mutu mumoja, kisha wakatwaa inchi yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.