Yeremia 35 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yeremia na wazao wa Rekabu

1Yawe akamutolea Yeremia ujumbe huu wakati wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:

2Kwenda kwa wazao wa Rekabu, useme nao. Kisha, uwalete katika chumba kimoja ndani ya nyumba yangu mimi Yawe, uwape divai wakunywe.

3Basi, nikamutwaa Yazania mwana wa Yeremia mujukuu wa Habazinia na wandugu zake pamoja na wanawake wote na ukoo wote wa Warekabu,

4nikawaleta kwenye nyumba ya Yawe, katika chumba cha wana wa mutu wa Mungu Hanani mwana wa Igidalia. Chumba hicho kilikuwa karibu na chumba cha wakubwa juu ya chumba cha mulinzi wa mulango Maseya mwana wa Salumu.

5Kisha nikaleta vikombe na mabakuli yaliyojaa divai mbele ya hao Warekabu, nikawaambia: Mukunywe divai.

6Lakini wao wakajibu: Sisi hatukunywi divai, maana Yonadabu mwana wa Rekabu, babu yetu, alituamuru hivi: Musikunywe divai; musikunywe ninyi wenyewe wala wana wenu milele.

7Musijenge nyumba, musilime mashamba, wala musikuwe na shamba la mizabibu. Lakini mutaishi katika mahema siku zote za maisha yenu, kusudi mupate kuishi siku nyingi katika inchi munamoishi kama wageni.

8Sisi tumeitii amri hiyo ya babu yetu Yonadabu mwana wa Rekabu siku zote, juu ya jambo alilotuamuru. Sisi hatukunywi divai hata kidogo; sisi wenyewe hatukunywi, wala wake zetu, wala watoto wetu wanaume au wanawake.

9Sisi hatujijengei nyumba za kuishi ndani yake. Hatuna mashamba ya mizabibu wala mashamba ya kulima na kupanda mbegu.

10Sisi tumeishi katika mahema na kutii mambo yote ambayo Yonadabu, babu yetu, alituamuru.

11Lakini Nebukadneza, mufalme wa Babeli alipofika, kuishambulia inchi hii, tuliamua kuja Yerusalema kwa kuepuka waaskari wa Wakaldea na wa Wasuria. Kwa hiyo sasa tunaishi katika muji Yerusalema.

12Kisha neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:

13Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwenda uwaambie watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema hivi: Ninyi hamuwezi kupokea mafundisho na kusikia maneno yangu?

–Ni ujumbe wa Yawe!

14Ile amri ambayo Yonadabu mwana wa Rekabu aliwapa wana wake kwamba wasikunywe divai, imefuatwa; nao hawakunywi divai mpaka siku hii ya leo, maana wametii amri ya babu yao. Lakini mimi nilisema nanyi tena na tena, nanyi hamukunisikiliza.

15Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.

16Wana wa Yonadabu mwana wa Rekabu wameshika amri waliyopewa na babu yao; lakini ninyi hamukunitii.

17Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninawaletea Wayuda na wakaaji wote wa Yerusalema hasara zote nilizosema juu yao, kwa sababu mimi nilisema nao, lakini hawakunisikiliza; niliwaita, lakini hawakuniitikia.

18Lakini Yeremia aliwaambia Warekabu hivi:

Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi Warekabu mumetii amri ya babu yenu, mukashika kanuni zake zote na kutenda kama alivyowaamuru.

19Kwa hiyo Yawe wa majeshi anasema hivi: Yonadabu mwana wa Rekabu hatakosa hata mara moja mutu wa uzao wake wa kunitumikia siku zote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help