1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Yawe ni kimbilio langu;
namna gani basi munaweza kuniambia:
“Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,
2maana waovu wanavuta pinde;
wameweka mishale tayari juu ya kamba,
kusudi wawapige mishale watu wenye moyo wa usawa katika giza!
3Kama misingi ikiharibiwa,
mutu wa haki atafanya nini?”
4Yawe yuko katika hekalu lake takatifu;
kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni.
Kwa macho yake anawachungulia wanadamu,
na kujua kila kitu wanachofanya.
5Yawe anawapima watu wa haki na waovu;
anawachukia wanaopenda kutesa kwa ukali.
6Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti;
upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.
7Yawe ni wa haki
na anapenda watu watende kwa haki.
Watu wa usawa wataona uso wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.