Mwanzo 42 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wandugu za Yosefu wanakwenda Misri

1Yakobo alipopata habari kwamba kulikuwa ngano kule Misri, akawaambia wana wake: “Mbona munaikaa mukiangaliana tu?

2Nimesikia kwamba Misri kuna ngano. Muende kule mununue ngano tusikufe na njaa.”

3Hivyo wandugu kumi za Yosefu wakaenda kwa kununua ngano.

4Lakini Yakobo hakumwacha Benjamina, ndugu ya Yosefu, aende pamoja nao maana aliogopa kwamba angeweza kupata hasara.

5Basi, wana wa Israeli wakafika Misri wakiwa kati ya wanunuzi wengine, maana hata katika inchi ya Kanana kulikuwa njaa.

6Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.

7Yosefu alipoona kaka zake akawatambua, lakini akajifanya sawa vile hawafahamu, akasema nao kwa ukali. Akawauliza: “Mumetoka wapi ninyi?”

Wakamujibu: “Tumetoka katika inchi ya Kanana, tumekuja kununua chakula.”

8Ingawa Yosefu aliwatambua kaka zake, wao hawakumutambua.

9Akakumbuka ndoto zake za zamani juu ya kaka zake, akawaambia: “Ninyi ni wapelelezi. Mumekuja kupeleleza uzaifu wa inchi yetu.”

10Wao wakamujibu: “Sivyo, bwana wetu. Sisi watumishi wako tumekuja kununua chakula.

11Sisi ni ndugu, wana wa baba mumoja. Sisi ni watu waaminifu, wala si wapelelezi.”

12Lakini Yosefu akawaambia: “Sivyo! Mumekuja hapa kwa kupeleleza uzaifu wa inchi yetu.”

13Wakamwambia: “Sisi, watumishi wako, tuko wandugu kumi na wawili, wana wa mutu mumoja, mwenyeji wa inchi ya Kanana. Mudogo wetu amebaki na baba kwa nyumba na ndugu yetu mwingine ni marehemu.”

14Lakini Yosefu akawaambia: “Ni kama vile nilivyosema: ninyi ni wapelelezi tu.

15Hivi ndivyo mutakavyojaribiwa: Ninaapa kwa jina la mufalme wa Misri, kwamba hamutatoka hapa mpaka mudogo wenu atakapokuja.

16Mutume mumoja wenu amulete yule ndugu yenu mudogo, wakati wengine wenu wanamungoja katika kifungo. Kwa hiyo ukweli wa maneno yenu utajulikana. Kama sivyo, ninaapa kwa jina la mufalme wa Misri kwamba ninyi ni wapelelezi.”

17Kisha akawatia wote katika kifungo kwa muda wa siku tatu.

18Siku ya tatu Yosefu akawaambia: “Kwa sababu ninamwogopa Mungu, mufanye hivi kusudi mupate kuishi:

19kama kweli ninyi ni watu waaminifu, mumoja wenu abaki katika kifungo na wengine wapeleke ngano kwa jamaa zenu wenye njaa.

20Kisha mumulete kwangu ndugu yenu mudogo. Hii itahakikisha ukweli wa maneno yenu, nanyi hamutauawa.”

Basi, wakakubali kufanya hivyo.

21Kisha wakasemezana wao kwa wao: “Kweli sisi tulimukosea ndugu yetu. Ingawa tulimwona katika taabu, hatukumujali hata alipotusihi. Ndiyo maana taabu hii yote inatupata.”

22Rubeni akawaambia: “Si niliwaambia tusimuzuru kijana? Lakini ninyi hamukunisikiliza! Sasa tunaazibiwa kwa ajili ya damu yake.”

23Wao hawakujua kwamba Yosefu alielewa yote yale waliyosema, maana alipoongea nao ilikuwa kwa njia ya mutafsiri.

24Yosefu akakwenda pembeni, akaanza kulia. Alipotulia, akarudi kuzungumuza nao. Kisha akamukamata Simeoni na kumufunga mbele ya macho yao.

Wandugu za Yosefu wanarudi kwao

25Yosefu akatoa amri wajaze mifuko yao na ngano na kumurudishia kila mumoja feza yake katika mufuko wake, na kuwapa chakula cha njia. Wakafanyiwa mambo hayo yote.

26Wakabebesha punda wao mizigo yao ya ngano, wakaondoka.

27Ikakuwa walipofika pahali pa kulala wageni kwa njia, mumoja wao akafungua mufuko wake kusudi apate kumukulisha punda wake, akashangaa kukuta feza yake kwenye kinywa cha mufuko wake.

28Akawaambia wandugu zake: “Feza yangu imerudishwa. Ndio hii hapa kwenye kinywa cha mufuko wangu!” Waliposikia hayo, wakavunjika moyo. Wakaangalia wakiwa wanatetemeka na kuulizana: “Ni jambo gani hili Mungu alilotutendea?”

29Walipofika katika inchi ya Kanana kwa baba yao Yakobo, wakamwelezea yote yaliyowapata, wakamwambia:

30“Mukubwa wa inchi ile alisema nasi kwa ukali, na kutuona kwamba sisi ni wapelelezi katika inchi yake.

31Lakini sisi tukamwelezea kwamba sisi ni watu waaminifu na wala si wapelelezi.

32Tukamwelezea kwamba sisi tuko wandugu kumi na wawili wa baba mumoja. Mumoja wetu ni marehemu na yule mudogo yuko kwetu katika inchi ya Kanana pamoja na baba yetu.

33Halafu mukubwa wa inchi hiyo akatuambia: ‘Hivi ndivyo nitakavyotambua kwamba kweli ninyi ni watu waaminifu. Muniachie kwangu ndugu yenu mumoja, nanyi wengine mupeleke ngano kwa jamaa zenu wenye njaa.

34Kisha muniletee yule ndugu yenu mudogo, na hapo nitajua kwamba ninyi si wapelelezi lakini ni watu waaminifu. Mukifanya hivyo nitamwacha huru ndugu yenu, nanyi mutaruhusiwa kufanya biashara katika inchi hii.’ ”

35Walipokuwa wanamimina ngano kutoka mifuko yao, wakashangaa kuona kila mumoja wao amerudishiwa kifuko chake na feza ndani ya mufuko wake. Walipoona hayo, wote pamoja na baba yao, wakashikwa na hofu.

36Baba yao Yakobo, akawaambia: “Munaniondolea watoto wangu! Yosefu hayuko, Simeoni hayuko, sasa munataka kumutwaa Benjamina. Hayo yote yanaanguka juu yangu!”

37Hapo Rubeni akamwambia baba yake: “Nisipomurudisha Benjamina, uwaue wana wangu wawili. Muache Benjamina katika mikono yangu, nami nitamulinda na kumurudisha kwako.”

38Lakini baba yake akamujibu: “Mwana wangu hatakwenda nanyi. Ndugu yake amekwisha kufa, naye peke yake ndiye aliyebaki. Mimi ni muzee mwenye imvi. Ikiwa kijana huyu atapatwa na hasara yoyote katika safari mutakayofanya basi, mutaniua kwa huzuni.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help