1Nilifikiri sana juu ya hayo yote, nikaona kwamba Mungu anaongoza matendo ya watu wenye hekima na wenye haki; ikiwa ni upendo au chuki, mwanadamu hajui. Kila kitu kwao ni bure,
2maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa.
3Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.
4Lakini anayeambatana na wanaoishi angali bado na tumaini. Afazali imbwa mwenye kuishi kuliko simba mwenye kufa.
5Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.
6Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua.
7Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.
8Vaa vizuri, ujipakae mafuta kwenye kichwa.
9Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.
10Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Hasara inakuja kwa rafla11Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.
12Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.
13Vilevile hapa chini ya jua nimeona mufano wa hekima, na ulionekana kwangu kuwa wenye maana sana.
14Kulikuwa muji mumoja mudogo wenye wakaaji wachache. Mufalme mumoja mwenye nguvu akafika, akauzunguka na kujitayarisha kuushambulia.
15Katika muji ule, kulikuwa masikini mumoja mwenye hekima ambaye, kwa hekima yake, aliokoa muji ule. Lakini hakuna mutu aliyemukumbuka yule masikini kisha.
16Basi, mimi ninasema, hekima ni bora kuliko nguvu, ingawa hekima ya masikini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.
17Afazali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima,
kuliko kusikiliza kelele za mufalme katika kikao cha wapumbafu.
18Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha,
lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.