Mika 6 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Malalamiko ya nabii

1Musikilize jinsi Yawe anavyosema:

Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima,

navyo vilima visikie sauti yako.

2Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima,

musikilize enyi misingi imara ya dunia!

Yawe yuko na maneno juu ya watu wake.

Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.

3Anasema hivi:

Enyi watu wangu, nimewatendea nini?

Nimewachokesha kwa kitu gani?

Munijibu!

4Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri,

niliwakomboa kutoka katika utumwa,

niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.

5Enyi watu wangu,

mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu,

na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu.

Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali.

Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!

6Nimwendee Yawe na kitu gani,

nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu?

Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto,

nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?

7Yawe atapendezwa

nikimutolea maelfu ya kondoo dume,

au mito elfu na elfu ya mafuta?

Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza

kwa ajili ya kosa langu,

mutoto wangu wa kwanza

kwa ajili ya zambi yangu?

Jibu la nabii

8Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu;

kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki:

kutenda mambo ya haki,

kupenda kuwa na huruma,

na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.

9Yawe anawaita wakaaji wa muji,

na ni jambo la hekima sana kumutii yeye:

Musikilize, enyi watu wa Yuda;

musikilize enyi muliokusanyika katika muji.

10Nitavumilia maovu

yaliyolundikwa ndani ya nyumba yao,

mali zilizopatikana kwa udanganyifu,

na matumizi ya vipimo vya udanganyifu,

jambo ambalo ni chukizo?

11Ninaweza kusema kwamba hawana kosa

watu wanaotumia vipimo vya udanganyifu

na mawe ya kupimia yasiyokuwa ya kweli?

12Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa,

wakaaji wake wanasema uongo,

kila neno wanalosema ni udanganyifu.

13Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini,

na kuwaangamiza kwa sababu ya zambi zenu.

14Mutakula lakini hamutashiba;

njaa itazidi kuwa katika tumbo yenu.

Mukiweka akiba haitachungwa,

na mukichunga kitu nitakiharibu kwa vita.

15Mutapanda mbegu, lakini hamutavuna.

Mutakamua mafuta ya zeituni, lakini hamutatumia mafuta hayo.

Mutakamua zabibu, lakini hamutakunywa divai hiyo.

16Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri

na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu,

na mumefuata mashauri yao.

Kwa hiyo nitawaletea maangamizi,

na kila mutu atawazarau.

Watu watawachekelea kila pahali.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help