1Yawe alinijaza uwezo wake mimi Ezekieli. Roho wake akanitwaa na kunipeleka katika bonde lililokuwa limejaa mifupa.
2Basi, akanitembeza kila pahali katika bonde lile. Kulikuwa mifupa mingi sana katika bonde lile, nayo ilikuwa inakauka kabisa.
3Yawe akaniuliza hivi: Wewe mwanadamu! Mifupa hii inaweza kuishi tena? Nami nikamujibu: Ee Bwana wetu Yawe, wewe unajua!
4Naye akaniambia: Toa unabii juu ya mifupa hii. Uiambie hivi: Enyi mifupa yenye kukauka, musikilize neno la Yawe.
5Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapulizia tena pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi.
6Nitawatia mishipa na nyama, nitawafunika ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi. Hapo mutajua kwamba mimi ni Yawe.
7Basi, nikatoa unabii kama nilivyoamriwa. Nilipokuwa nikitoa unabii, kukatokea kelele kama ya mukwaruzo na ile mifupa ikaanza kusogeleana na kuungana.
8Niliangalia, nikaona ile mifupa imewekewa mishipa na nyama na kufunikwa kwa ngozi. Lakini haikukuwa na uzima.
9Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.
10Basi, mimi nikatoa unabii kama alivyoniamuru, nayo pumzi ikaingia ndani yao, nayo ikapata tena uzima, ikasimama wima: kundi kubwa ajabu.
11Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.
12Kwa hiyo, toa unabii, uwaambie kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu. Nitawarudisha ndani ya nyumba zenu katika inchi ya Israeli.
13Nanyi, enyi watu wangu, mutatambua kwamba mimi ni Yawe nitakapofunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu.
14Nitatia Roho yangu ndani yenu, nanyi mutaishi, nami nitawaweka katika inchi yenu wenyewe. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi Yawe nimesema, nami nitafanya hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
15Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
16Wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja, uandike juu yake maneno haya: Kwa Yuda na Waisraeli wanaoshirikiana naye. Kisha twaa kijiti kingine uandike juu yake maneno haya: Kwa Yosefu (kijiti cha Efuraimu) na Waisraeli wanaoshirikiana naye.
17Halafu uvitwae vijiti hivyo na kuvishikamanisha kusudi vionekane kama kijiti kimoja.
18Wanainchi wenzako watakuuliza: Hautatuelezea maana ya jambo hilo?
19Wewe utawajibu: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakitwaa kijiti cha Yosefu (kinachokuwa katika mukono wa Efuraimu) na makabila ya Israeli yanayoungana naye, nami nitakishikamanisha na kijiti cha Yuda kusudi vijiti hivyo viwili vifanywe kijiti kimoja katika mukono wangu.
20Utakamata vile vijiti ulivyoandika juu yake katika mukono wako kwa jinsi kila mutu apate kuona,
21uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika inchi yao.
22Nitawafanya kuwa taifa moja katika inchi juu ya milima ya Israeli; mufalme mumoja atakuwa mufalme wao wote. Hawatakuwa tena mataifa mawili wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.
23Hawatajichafua tena kwa kuabudu sanamu za miungu yao na kwa mambo yao ya kuchukiza wala kwa makosa yao. Nitawaokoa wasikuwe tena waasi. Nao watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
24Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao; watakuwa na muchungaji mumoja tu. Watayafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu.
25Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.
26Nitafanya nao agano la amani, nalo litakuwa agano la milele. Nitawabariki na kuwafanya wakuwe wengi, nami nitaweka hekalu langu kati yao milele.
27Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.
28Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi Yawe, nimewatakasa Waisraeli na kwamba hekalu langu liko kati yao milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.