Zaburi 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

SEHEMU YA KWANZA(Zaburi 1–41)

1Heri mutu asiyefuata shauri la waovu,

asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi,

wala kukusanyika na wenye kuzarau;

2lakini anafurahia sheria ya Yawe,

na kuifikiri muchana na usiku.

3Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito,

unaozaa matunda kwa wakati wake,

na majani yake hayanyauki hata kidogo.

Anafanikiwa katika yote anayofanya.

4Lakini waovu si vile hata kidogo.

Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.

5Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,

wenye zambi hawatashiriki katika kusanyiko la watu wa haki.

6Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki;

lakini njia ya waovu itaangamia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help