1Haya ni maono ya Obadia.
Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu.
Yawe ataazibu taifa la EdomuTumepata habari kutoka kwa Yawe;
mujumbe ametumwa kati ya mataifa:
Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!
2Yawe aliambia taifa la Edomu:
Nitakufanya kuwa mudogo kati ya mataifa,
utazarauliwa kabisa na wote.
3Kiburi chako kimekudanganya:
wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa
na makao yako yapo juu kwenye milima,
hivyo unajisemesha:
Nani anayeweza kunishusha chini?
4Hata ukiruka juu kama tai,
ukifanya makao yako kati ya nyota,
mimi nitakushusha chini tu.
–Ni ujumbe wa Yawe.
5Kama wizi au wanyanganyi wangekufikia usiku,
si wao wangekuiba tu vitu wanavyokuwa navyo lazima?
Ikiwa wavunaji wa zabibu wangekufikia,
si wangekuachia sehemu ndogo tu?
Lakini wewe, waadui zako wamekuangamiza kabisa.
6Enyi wazao wa Esau, mali yenu imenyanganywa,
akiba zenu zote zilizofichwa zimevumbuliwa!
7Washirika wenzenu wamewadanganya,
wamewafukuza toka katika inchi yenu.
Watu muliopatana nao wamewashinda katika vita.
Warafiki wa kutegemewa ndio waliokutegea mitego,
nawe haukuelewa yaliyokuwa yanatendeka.
8Mimi Yawe ninakuuliza hivi:
Siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu
na wenye maarifa kutoka mulima wa wazao wa Esau?
9Ewe muji wa Temani, mashujaa wako wataogopa
na kila mutu juu ya mulima wa wazao wa Esau.
Sababu za kuazibiwa kwa taifa la Edomu10Kwa sababu ya mateso makali
muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo,
mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.
11Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu,
wakati wageni walipouteka utajiri wao,
walipoingia katika milango yake
na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura.
Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.
12Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu,
hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa,
hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,
13hamukupaswa kuingia katika muji wa watu wangu, siku walipopatwa na hasara,
hamukupaswa kukamata mali zao, siku hiyo ya hasara yao,
14hamukupaswa kusimama kwenye masanganjia na kuwakamata wakimbizi wao,
hamukupaswa kuwatoa kwa waadui zao wale waliobaki wazima.
Mungu atayahukumu mataifa15Siku inakaribia ambapo mimi Yawe
nitayahukumu mataifa yote.
Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa,
mutalipwa kulingana na matendo yenu.
16Maana, kama walivyokunywa kikombe cha kasirani yangu
kwenye mulima wangu mutakatifu,
ndivyo mataifa jirani watakavyokunywa;
watakunywa na kupepesuka,
wataangamia na kuwa kama hawakukuwa mbele katika dunia.
Waisraeli watashinda17Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni
nao utakuwa mulima mutakatifu.
Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao
toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.
18Wazao wa Yakobo watakuwa kama moto
na wazao wa Yosefu kama ndimi za moto.
Watawaangamiza wazao wa Esau
kama vile moto unavyoteketeza majani yenye kukauka,
hakutaponyoka hata mumoja wao.
–Yawe amesema.
19Wale wanaokaa Negebu wataurizi mulima wa wazao wa Esau,
wale wanaokaa katika Shefela watarizi inchi ya Wafilistini.
Waisraeli watarizi inchi za Efuraimu na Samaria
na watu wa kabila la Benjamina watarizi inchi ya Gileadi.
20Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho,
lile jeshi la Waisraeli,
watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata.
Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi
watarizi miji ya Negebu.
21Wakombozi watapanda juu ya mulima Sayuni
kwa kuutawala mulima wa wazao wa Esau;
naye Yawe atakuwa ndiye Mufalme.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.