ZAKARIA 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuanguka kwa wenye nguvu

1Fungua milango yako, ewe Lebanoni

kusudi moto uiteketeze mierezi yako!

2Muomboleze, enyi misunobari,

kwa sababu mierezi imeteketea.

Miti hiyo mitukufu imeharibiwa!

Enyi mialo ya Basani, muomboleze,

kwa maana pori kubwa limekatwa!

3Sikia maombolezo ya watawala!

Utukufu wao umeharibiwa!

Sikia ngurumo za simba!

Pori la muto Yordani limeharibiwa!

Wachungaji wawili

4Yawe, Mungu wangu, alisema hivi: Ujifanye muchungaji wa kondoo wanaokwenda kuchinjwa.

5Wanunuzi wao wanawachinja lakini hawaazibiwi; na wanaowauzisha wanasema: “Yawe ashukuriwe! Sasa tumetajirika.” Hata wachungaji wenyewe hawawaonei huruma.

6Sitawahurumia tena wakaaji wa dunia. Nitamwacha kila mutu katika mikono ya mwenzake, na kila mwanainchi katika mikono ya mufalme wake. Nao wataiangamiza dunia, nami sitamwokoa mutu yeyote toka katika mikono yao.

–Ni ujumbe wa Yawe.

7Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.

8Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.

9Basi, nikawaambia: “Sitakuwa muchungaji wenu tena. Atakayekufa akufe! Atakayeangamia aangamie! Na wale watakaobaki wakulane wao kwa wao.”

10Nikakamata ile fimbo yangu niliyoiita “Rehema”, nikaivunja, kuonyesha kwamba agano Yawe alilofanya na watu wake limevunjwa.

11Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.

12Kisha nikawaambia: Kama mukipendezwa, munilipe mushahara wangu; lakini kama munaona sivyo, basi muache. Basi, wakanipimia vikoroti makumi tatu vya feza kwa mushahara wangu. Hivyo nikatwaa hivyo vikoroti makumi tatu vya feza, nikavitia katika hazina ya hekalu la Yawe.

14Kisha nikavunja ile fimbo yangu ya pili niliyoiita “Umoja” na hivyo nikauvunja umoja kati ya Yuda na Israeli.

15Yawe akaniambia tena: Ujifanye tena kuwa muchungaji, lakini mara hii ukuwe kama muchungaji mupumbafu!

16Maana nitaleta katika inchi muchungaji asiyemujali kondoo anayeangamia, au kumutafuta kondoo anayetangatanga, au kumutunza aliyeumizwa wala kumukulisha yule anayekuwa muzima: lakini atakula wale kondoo wanono, hata kwato zao.

17Ole wake muchungaji mupumbafu,

ambaye anawaachilia kondoo wake!

Upanga uukate mukono wake,

na jicho lake la kuume liongolewe!

Mukono wake upooze,

jicho lake la kuume lipofuke.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help