Matayo 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yesu na siku ya Sabato(Mk 2.23-28; Lk 6.1-5)

1Katika siku zile Yesu akapita katika mashamba ya ngano kwa siku moja ya Sabato. Wanafunzi wake wakasikia njaa; kwa hiyo wakaanza kuchumachuma masuke ya ngano na kuyakula.

2Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakamwambia Yesu: “Angalia! Wanafunzi wako wanafanya mambo yanayokatazwa kufanya kwa siku ya Sabato!”

3Yesu akawajibu: “Hamujasoma bado vile Daudi alivyofanya wakati yeye pamoja na watu wake waliposikia njaa?

4Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate mitakatifu iliyotolewa kwa Mungu. Ijapokuwa vile haikuruhusiwa kwake wala kwa watu wake kukula mikate kama ile, isipokuwa makuhani peke yao.

5Vilevile hamujasoma bado katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba kila siku ya Sabato, makuhani wanaotumika ndani ya hekalu wanavunja Sheria inayoelekea siku ile, nao hawahesabiwi kuwa na kosa?

6Lakini sasa ninawaambia kama hapa kuna mukubwa kupita hekalu!

7Mungejua maana ya Maandiko haya Matakatifu, yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu,’ hamungehukumu watu hawa wasiokuwa na kosa.

8Kwa maana Mwana wa Mutu ndiye Bwana wa siku ya Sabato.”

Mutu mwenye mukono unaokauka(Mk 3.1-6; Lk 6.6-11)

9Yesu akaondoka ngambo za kule, na kwenda ndani ya nyumba moja ya kuabudia.

10Mule ndani mulikuwa mutu mumoja mwenye mukono unaokauka. Nao watu wamoja waliokuwa pale walitafuta sababu ya kumushitaki Yesu; kwa hiyo wakamwuliza: “Sheria yetu inaruhusu kumuponyesha mutu kwa siku ya Sabato?”

11Yesu akawajibu: “Kama mutu mumoja kati yenu akiwa na kondoo mumoja, na kondoo yule akitumbukia ndani ya shimo kwa siku ya Sabato, hatamukamata na kumwondosha mule siku ile ile?

12Naye mutu ni wa lazima kuliko kondoo! Basi Sheria inaturuhusu kutenda mema kwa siku ya Sabato.”

13Kisha Yesu akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Naye akaunyoosha, nao ukakuwa tena muzima sawa ule mwingine.

14Wafarisayo wakaondoka pale na kwenda kufanya shauri la kumwua Yesu.

Mutumishi Mungu aliyejichagulia

15Yesu alipojua habari ile, akaondoka kule. Watu wengi wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa wote.

16Akawaagiza wasimutambulishe kwa watu.

17Ilitokea vile kusudi yatimie maneno haya Mungu aliyoyasema kwa njia ya nabii Isaya:

18“Muangalie, mutumishi wangu niliyejichagulia,

anayekuwa mupendwa wangu, ninayependezwa naye.

Nitamujaza Roho wangu,

naye atatangaza haki yangu kwa mataifa.

19Hatabishana wala kupiga kelele,

wala hakuna atakayesikia sauti yake katika barabara.

20Hatavunja tete linalokunja,

wala hatazimisha taa inayofifia,

mpaka aiwezeshe haki kutawala.

21Nayo mataifa yote yatamutumainia.”

Yesu anashitakiwa kuwa Belzebuli(Mk 3.22-30; Lk 11.14-23)

22Kisha wakamuletea Yesu mutu mumoja aliyeshikwa na pepo, aliyemufanya kuwa kipofu na bubu. Yesu akamuponyesha mutu yule hata akaanza kusema na kuona.

23Na kundi lote la watu waliokuwa pale wakashangaa na kusema: “Huyu anaweza kuwa kweli Mwana wa Daudi?”

24Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”

25Yesu akitambua mafikiri yao, akawaambia: “Watu wa ufalme wowote wakigombana wao kwa wao, ufalme ule utaanguka. Nao wakaaji wa muji wowote au watu wa jamaa yoyote wakigombana wao kwa wao, muji ule au jamaa ile haitadumu.

26Na kama Shetani akimufukuza Shetani anajigombanisha yeye mwenyewe, nao ufalme wake utaanguka.

27Ninyi munasema kwamba ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli. Basi watu wa kikundi chenu wanawafukuza kwa uwezo wa nani? Watu hao wanashuhudia kwa njia ya matendo yao kwamba ninyi ni wakosaji!

28Kwa ngambo yangu ninafukuza pepo kwa uwezo wa Roho wa Mungu. Hii inaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha kufika kati yenu.

29“Hakuna mutu anayeweza kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kunyanganya vitu vyake, isipokuwa kwanza anamufunga. Na kisha anaweza kunyanganya vitu vyake vyote.

30“Asiyekuwa wa upande wangu ni adui yangu; na asiyekusanya pamoja nami, anasambaza.

31Kwa hiyo ninawaambia: watu wataweza kusamehewa zambi zote wanazofanya na matusi yao yote. Lakini mutu anayetukana Roho Mutakatifu hatasamehewa.

32Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.

Muti na matunda yake(Lk 6.43-45)

33“Muti ukiwa muzuri, matunda yake yatakuwa mazuri vilevile; nao muti ukiwa mubaya, matunda yake yatakuwa mabaya vilevile. Kwa maana muti unatambulikana kwa matunda yake.

34Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.

35Mutu muzuri anatwaa vitu vizuri toka ndani ya akiba yake nzuri, naye mutu mubaya anatwaa vitu vibaya toka ndani ya akiba yake mbaya.

36“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.

37Kwa maana kila mutu atapata sheria au kupata azabu kufuatana na maneno yake.”

38Halafu walimu wamoja wa Sheria na Wafarisayo wamoja wakamwambia Yesu: “Mwalimu, tunataka kuona kitambulisho toka kwako.”

Wafarisayo wanataka kitambulisho(Mk 8.11-12; Lk 11.29-32)

39Yesu akawajibu: “Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu, wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataona kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.

40Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.

41Kwa Siku ya hukumu, watu wa Ninawe watasimama nanyi watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu wao waligeuka toka zambi zao waliposikia mahubiri ya Yona. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Yona!

42Vilevile kwa Siku ya hukumu malkia toka kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikia maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kumupita Solomono!

Yanayotokea wakati pepo wanapomurudilia mutu(Lk 11.24-26)

43“Wakati pepo imekwisha kutoka ndani ya mutu, inazungukazunguka katika jangwa kutafuta nafasi ya kupumzikia. Naye asipopata nafasi ile,

44anasema: ‘Nitarudi ndani ya nyumba yangu nilimotoka.’ Anaporudi, anaikuta wazi bila kitu, nayo imefagiliwa na kupambwa vizuri.

45Halafu anakwenda kutwaa pepo wengine saba wanaokuwa wabaya kumupita, nao wote wanakuja kuingia na kukaa mule. Na hali ya mwisho ya mutu yule inageuka mbaya kuliko hali yake ya kwanza. Na hivi ndivyo itakavyokuwa kwa watu wa kizazi hiki kibaya.”

Mama na wandugu za Yesu(Mk 3.31-35; Lk 8.19-21)

46Yesu alipokuwa hajamaliza kusema na lile kundi la watu, mama yake na wandugu zake wakafika. Walisimama inje wakitaka kusemezana naye.

47Halafu mutu mumoja akamwambia: “Angalia, mama yako na wandugu zako wako inje; wanataka kusemezana nawe.”

48Yesu akamujibu mutu yule: “Ni nani ndiye mama yangu, na nani ndio wandugu zangu?”

49Kisha akawanyooshea wanafunzi wake mukono, na kusema: “Angalia, hawa ndio mama yangu na wandugu zangu.

50Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help