1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa watu wa Gati: Zaburi ya Wakora.
2Ee Yawe wa majeshi,
kweli makao yako yanapendeza!
3Nafsi yangu inatamani sana hekalu la Yawe!
Moyo na mwili wangu wote vinamushangilia Mungu Mwenye Uzima.
4Karibu na mazabahu zako,
ee Yawe wa majeshi, mufalme wangu na Mungu wangu,
hata kichororo ana makao yake,
naye mbaruwayi amejenga chicha yake ambamo anaweka vitoto vyake,
5Heri wale wanaokaa ndani ya nyumba yako,
wakiimba sifa zako siku zote.
6Heri watu wanaopata nguvu zao kwako,
wanaotamani kusafiri kwa kuabudu kwa mulima wako.
7Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka,
wanalifanya kuwa chemichemi,
nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.
8Wanaendelea wakipata nguvu zaidi na zaidi:
watamwona Mungu wa miungu huko Sayuni.
9Usikie maombi yangu, ee Yawe, Mungu wa majeshi!
Unitegee sikio, ee Mungu wa Yakobo.
10Ee Mungu,
umwangalie huyo ngao yetu,
upendezwe na huyo uliyemuchagua.
11Siku moja tu ndani ya hekalu lako,
ni bora kuliko siku elfu pahali pengine;
afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako,
kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.
12Yawe Mungu ni jua na ngao yetu.
Anatukubali na anatupatia utukufu.
Hawanyimi kitu chochote kizuri
wale wanaoishi katika ukamilifu.
13Ee Yawe wa majeshi,
heri mutu yule anayekutumainia wewe!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.