Zaburi 78 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu na watu wake

1Mashairi ya Asafu.

Musikie mafundisho yangu, enyi watu wangu,

mutegee sikio maneno ya kinywa changu.

2Nitasema nanyi kwa mafumbo,

nitasema mambo yaliyofichwa tangu zamani;

3mambo tuliyosikia na kuyajua,

mambo ambayo babu zetu walituelezea.

4Hatutayaficha kwa watoto wetu

lakini tutawaelezea kizazi kinachokuja

matendo ya utukufu ya Yawe na uwezo wake;

tutawaambia maajabu yake aliyotenda.

5Aliwapa wazao wa Yakobo masharti,

aliweka sheria katika Israeli

ambayo aliwaamuru babu zetu

wawafundishe watoto wao;

6kusudi watu wa kizazi kinachokuja,

watoto watakaozaliwa kisha, wazijue,

nao pia wawajulishe watoto wao,

7kusudi wamwekee Mungu tumaini lao,

wasipate kusahau matendo ya Mungu,

lakini washike amri zake,

8wasikuwe kama vile babu zao walivyokuwa,

watu wagumu na waasi,

kizazi ambacho hakikuwa na musimamo kamili,

ambacho hakikuwa na uaminifu kwa Mungu.

9Watu wa Efuraimu, pinde na mishale katika mukono,

walirudi nyuma, wakakimbia siku ile ya vita.

10Hawakushika agano la Mungu;

walikataa kufuata sheria yake.

11Walisahau mambo aliyokuwa ametenda,

ndiyo miujiza aliyokuwa amewaonyesha.

12Alifanya maajabu mbele ya babu zao,

katika mbuga za Soani kule Misri.

13Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake;

aliyafanya maji yasimame kama ukuta.

14Muchana aliwaongoza kwa wingu;

usiku kucha kwa mwangaza wa moto.

15Alipasua mawe kule katika jangwa,

akawakunywesha maji kutoka shimo refu.

16Alitiririsha vijito kutoka katika jiwe,

nayo maji kama mito.

17Hata hivyo waliendelea kumukosea Mungu;

walimwasi Mungu Mukubwa kule katika jangwa.

18Walimujaribu Mungu kwa makusudi;

wakidai wapewe chakula walichotaka.

19Walimutukana Mungu wakisema:

“Hakika, Mungu anaweza kutupatia chakula katika jangwa?

20Ni kweli, alipiga jiwe,

maji yakatiririka kama muto;

lakini, sasa anaweza kweli kutupatia mukate,

na kuwapatia watu wake nyama?”

21Yawe, aliposikia hayo,

akakasirika,

moto ukawawakia wazao wa Yakobo,

hasira yake ikapanda juu ya watu wa Israeli,

22kwa sababu hawakumwaminia,

wala hawakutumainia kwamba angeweza kuwaokoa.

23Hata hivyo aliamuru mawingu,

akafungua milango ya mbingu;

24akawanyeshea mana wapate kula,

akawapa ngano kutoka mbinguni.

25Wanadamu wakakula chakula cha wamalaika;

naye aliwapelekea chakula cha kutosha.

26Alivumisha upepo wa mashariki,

kwa nguvu yake akachochea upepo wa kusini,

27akawaangushia watu wake nyama kama vumbi,

ndege wengi kama muchanga wa bahari.

28Ndege hao walianguka katika kambi lao,

kandokando ya makao yao.

29Watu walikula wakashiba;

Mungu aliwapa walichotaka.

30Lakini mbele ya kukata hamu yao,

chakula kilipokuwa kingali katika kinywa,

31hasira ya Mungu iliwaka juu yao;

akaua wenye nguvu kati yao,

na kuwaangusha vijana wa Israeli.

32Hata hivyo waliendelea kumukosea Mungu;

ijapokuwa alitenda maajabu, hawakuamini.

33Basi, akatowesha siku zao kama pumzi,

miaka yao kwa misiba ya rafla.

34Kila mara alipowaua, waliobaki walimugeukia;

wakageuka toka ubaya wao, wakamugeukia Mungu kwa moyo.

35Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa kikingio chao,

kwamba Mungu Mukubwa alikuwa mukombozi wao.

36Lakini walimudanganya kwa maneno yao;

walimwambia uongo.

37Hawakuambatana naye kwa moyo,

hawakukuwa waaminifu kwa agano lake.

38Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao,

wala hakuwaangamiza.

Mara nyingi alizuia hasira yake,

wala hakuacha kasirani yake yote iwake.

39Alikumbuka kwamba wao ni watu tu;

ni kama upepo unaopita na kutoweka.

40Mara ngapi walimwasi kule katika jangwa,

na kumuchukiza huko kwenye ukiwa!

41Walimujaribu Mungu tena na tena,

wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.

42Hawakukumbuka nguvu yake,

wala siku ile alipowaokoa kutoka waadui zao,

43alipotenda maajabu katika inchi ya Misri,

na miujiza katika mbuga za Soani!

44Aligeuza ile mito kuwa damu,

Wamisri wasipate maji ya kunywa.

45Aliwapelekea makundi ya mainzi yaliyowasumbua,

na vyura waliowaletea hasara.

46Alituma nzige, wakakula mavuno yao,

na kuharibu mashamba yao.

47Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe,

na mitini yao kwa baridi kali.

48Ngombe wao aliwaua kwa mvua ya mawe,

na kondoo wao kwa radi.

49Alimwanga juu yao hasira yake kali,

kasirani, chuki na taabu,

na kuwashushia kundi la wamalaika waangamizaji.

50Aliachilia hasira yake iendelee,

wala hakuwaepusha na kifo,

lakini aliwaangamiza kwa ugonjwa mukali.

51Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri;

ndilo chipukizi la kwanza katika kambi la Hamu.

52Kisha aliwahamisha watu wake kama kondoo,

akawaongoza katika jangwa kama kundi la nyama.

53Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa;

lakini bahari iliwafunika waadui zao.

54Aliwaleta katika inchi yake takatifu,

katika mulima aliounyanganya kwa nguvu yake.

55Alifukuza mataifa mbele yao,

akatoa inchi zao zikuwe mali ya Israeli,

akaikalisha makabila ya Israeli katika mahema zao.

56Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa;

wala hawakushika maagizo yake.

57Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao;

wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.

58Walimukasirikisha kwa mazabahu zao za miungu;

wakamutia wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.

59Mungu alipoona hayo, akawaka hasira;

akamukataa Israeli kabisa.

60Aliacha makao yake kule Shilo,

makao ambamo alikaa kati ya watu.

61Aliacha kitambulisho cha nguvu yake kinyanganywe,

utukufu wake utiwe katika mikono ya waadui.

62Aliwakasirikia watu wake mwenyewe;

akawatoa waangamizwe kwa upanga.

63Moto ukawateketeza vijana wao wanaume,

na wabinti wao wakakosa wachumba.

64Makuhani wao walikufa kwa upanga,

wala wajane wao hawakuomboleza.

65Kisha Bwana aliamuka kama kutoka katika usingizi,

kama shujaa aliyechangamushwa na divai.

66Akawashinda waadui zake;

akawafezehesha kwa milele.

67Alikataa wazao wa Yosefu,

wala hakuchagua kabila la Efuraimu.

68Lakini alichagua kabila la Yuda,

mulima Sayuni anaoupenda.

69Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu,

kama dunia aliyoiimarisha milele.

70Alimuchagua Daudi, mutumishi wake,

akamutoa katika kazi ya kuchunga kondoo.

71Alimutoa katika kazi ya kuchunga kondoo na wana-kondoo,

akuwe na madaraka ya kuchunga watu wa Yakobo taifa lake,

achunge Israeli, watu wa pekee wa Mungu.

72Daudi akawafundisha kwa moyo mukamilifu,

akawaongoza kwa uhodari mukubwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help